Mstaafu kutoka Wizara ya Kilimo, Daniel Shigela na mkewe wamekabidhiwa sh milioni tano kutoka kwenye bahati nasibu ya biko inayoendesha bahati nasibu nchini, huku ikitoa fursa za Watanzania kuibuka mamilionea kwa kushinda kwenye mchezo huo.

Makabidhiano hayo yamefanyika mkoani Arusha, akiwa sambamba na mkewe Edith Shigela ikiwa ni siku moja tu baada ya kushinda.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Shigela aliishukuru Biko kwa kumpatia fedha zake hizo akisema kuwa fedha hizo zitawanufaisha yeye na mkewe kwenye familia yao hiyo.

Kucheza Biko sasa ni kuanzia sh 500 na sh 1000 na kuendelea, huku ushindi wake ukianzia sh 1000 hadi sh 100000 kwa watakaocheza sh 500 hadi sh 9500 wakati  watakaocheza kwa sh 1000 na kuendelea, mchezaji anaweza kujishindia zawadi ya papo kwa hapo kuanzia sh 5000 hadi sh milioni moja bila kusahau wote kuingia kwenye droo kubwa ya Jumatano na Jumapili.

Bahati nasibu ya Biko inachezwa kwa mitandao ya simu minne ambayo ni Tigo Pesa, M-Pesa, Artel Money na HaloPesa, ambapo namba ya Kampuni ni 505050 na kumbukumbu namba 2456, huku Watanzania wakiweza kujishindia zawadi kubwa katika droo ya Jumatano na Jumapili

 Mstaafu kutoka Wizara ya Kilimo, Daniel Shigela, mwenye maskani yake Sombetini jijini Arusha, akiwa na nyuso ya furaha na mke wake Edith Shigela baada ya kukabidhiwa fedha zao sh milioni tano alizoshinda kutoka kwenye bahati nasibu ya Biko inayondelea kumwaga mamilioni kwa Watanzania wanaocheza Biko mchezo huo ambapo sasa droo ya wapendanao ikichezeshwa na watu kuvuna fedha pamoja na bodaboda. Picha na Mpigapicha Wetu.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...