Mstaafu
kutoka Wizara ya Kilimo, Daniel Shigela na mkewe wamekabidhiwa sh
milioni tano kutoka kwenye bahati nasibu ya biko inayoendesha bahati
nasibu nchini, huku ikitoa fursa za Watanzania kuibuka mamilionea kwa
kushinda kwenye mchezo huo.
Makabidhiano hayo yamefanyika mkoani Arusha, akiwa sambamba na mkewe Edith Shigela ikiwa ni siku moja tu baada ya kushinda.
Akizungumza
katika makabidhiano hayo, Shigela aliishukuru Biko kwa kumpatia fedha
zake hizo akisema kuwa fedha hizo zitawanufaisha yeye na mkewe kwenye
familia yao hiyo.
Kucheza
Biko sasa ni kuanzia sh 500 na sh 1000 na kuendelea, huku ushindi wake
ukianzia sh 1000 hadi sh 100000 kwa watakaocheza sh 500 hadi sh 9500
wakati watakaocheza kwa sh 1000
na kuendelea, mchezaji anaweza kujishindia zawadi ya papo kwa hapo
kuanzia sh 5000 hadi sh milioni moja bila kusahau wote kuingia kwenye
droo kubwa ya Jumatano na Jumapili.
Bahati
nasibu ya Biko inachezwa kwa mitandao ya simu minne ambayo ni Tigo
Pesa, M-Pesa, Artel Money na HaloPesa, ambapo namba ya Kampuni ni 505050
na kumbukumbu namba 2456, huku Watanzania wakiweza kujishindia zawadi
kubwa katika droo ya Jumatano na Jumapili
Mstaafu kutoka Wizara ya Kilimo, Daniel Shigela, mwenye maskani yake Sombetini jijini Arusha, akiwa na nyuso ya furaha na mke wake Edith Shigela baada ya kukabidhiwa fedha zao sh milioni tano alizoshinda kutoka kwenye bahati nasibu ya Biko inayondelea kumwaga mamilioni kwa Watanzania wanaocheza Biko mchezo huo ambapo sasa droo ya wapendanao ikichezeshwa na watu kuvuna fedha pamoja na bodaboda. Picha na Mpigapicha Wetu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...