Waziri wa Mifugo naUvuvi Mh. Luhaga Joelson Mpina(mwenye mkasi) akikata utepe wa Ofisiya TAFICO katika uzinduzi rasmi wa ofisi na Menejimenti ya mpito ya kusimamia hatua za kufufua TAFICO Menejimenti hiyo ilizinduliwa  Julai 1/2018,anayefuata ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumuya Bunge ya Kilimo Mifugo na Maji, Mheshimiwa MahamoudMgimwa wa kwanza kuliani Kaimu Meneja Mkuu wa TAFICO Esther Mndeme. 
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh. Luhaga Joelson Mpina akitoa hotuba yake wakati wa uzinduzi rasmi wa ofisi na Menejimenti ya mpito ya kusimamia hatua za kufufuaTAFICOMenejimenti hiyo ilizinduliwa na tarehe 01/07/2018; kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo Mifugo na Maji, Mheshimiwa MahamoudMgimwa. 


Ataka zilizo baki zisalimishwe kwa hiari haraka.
· Asisitiza kuendelea kuzisaka nchi nzima 

NA JOHN MAPEPELE, DODOMA

WIZARA ya Mifugo na Uvuvi imetaifish amali za Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) zenye thamani ya shbilioni 118 zilizokuwa zinamilikiwa nawat ukinyemela kisha kuzirejesha serikalini ikiwa ni miongoni mwa mikakati ya Serikali ya awamu ya tano ya kulifufua shirika hilo. 

Zoezi hilo limefanyika katika kipindi cha ndaniyasiku 30 

Pia Serikali inaendelea na uhakiki wa mali hizo popote zilizopo ambazo na zozote zitarejeshwa ili kuwezesha shirika hilo kuanza kazi baada ya menejimenti yake kuundwa mwishoni mwa mwaka jana. 

Akijibu hoja za wabunge kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Kamati ya Kudumu ya Bunge Kilimo, Mifugo na Maji bungeni mjini Dodoma, Waziri wa Mifugo naUvuvi, Luhaga Mpina Serikali ya awamu ya tano iko kwenye hatua za mwisho za kulifufuashirikahilo. 

Pia Serikali inajiandaa kununua meli mbili kubwa ambazo zifanya kazi ya uvuvi katika ukanda wa uchumi wa bahari kuu ilikukidhi matakwa ya wabunge ambao kwa miaka mingi wamekuwa wakiitaka Serikali kuwekeza kwenye ukanda huo. 

AidhaWaziri MpinaalisematayariSerikaliya apanimeshaahidikutoashbilioni 4.3 kwaajiliyakufufuamiundombinuyaShirika la Uvuvi ikiwemomajokofuyakuhifadhisamaki, gari la barafu, melimojayauvuvinakujengagati la kuegeshameli za shirikahilo. 

“Kumekuwa na kilio cha wabunge cha miaka mingi kutakaSerikali iingie kwenye uvuvi wa bahari kuu,nataka kuwahakikishia Serikali ya awamu yatano tunaingia kuvua kwenye uvuvi wa bahari kuu na mipango iko vizuri”alisemaMpina 

Kuhusu ujenzi wa bandari yaUvuvi, Waziri Mpina alisema tayari mtaalamu mwelekezi anaendelea na kazi ya upembuzi yakinifu na kwamba mara baada ya kukamilika kazi hiyo ujenzi wa bandari ya uvuvi utaanza . 

Waziri Mpina amesisiti za kuwa mbali nakulifufua shirika la uvuvi, Serikali ya awamu ya tano inakwenda kufufua viwanda vya kuchakata mazao ya mifugo nakujenga vingine vipya katika maeneo mbalimbali nchini. 

“Hivi sasa ujenzi wakiwanda kikubwa cha kuchakata mazao ya mifugo kinakwenda kujengwa eneo la Ruvu ambacho kitakuwa na machinjio ,kitasindikanyama, kitasindikangozi, kitasindika mazao ya ngozi ukiingiza mfugo unatokana kiatu”alisemaMpina 

Alisema, tayariWizaraimefanyamkutanotarehe 5/2/2019 naujumbewa Waziri waKilimona Ardhi waMisriMheshimiwa, DktEzzidine Abu Stiet, ulioongozwanaBaloziwaMisrinchiniMheshimiwa, Mohammed Gaber Abdulwafa. 

“Tumekubaliana kuwa, utiaji wa saini mkataba huo utafanyika tarehe 24/2/2019 hapa nchini. Baina ya Kampuni ya Ranchi za Taifa(NARCO) kwa upande wa Tanzania na Kampuni ya Uwekezaji kwa Nchi za Afrika ya nchini Misri ijulikanayo kama “The National Egyptian Company for Africa Investment” (NECAI) kwa niaba ya Serikali ya Misri” alisisitiza 

Pia Serikali itaanza ujenzi wa mnada wa kimataifa wa mifugo Ruvu na kwamba tayari wamekutanana Waziri waMifugo wa Misri kukubaliana ujenzi wa kiwanda hicho uanze Machi mwaka huu. 

Vile vile viwanda vingine vya kuchakat amazao ya mifugo vinajengwa Longido, Tan Choice Kibaha chenye uwezo wa kuchinja ngombe zaidi 1,000 na mbuzi 4,000 nakiko kwenye hatua ya mwisho kukamilishwa huku Kampuniya KOMU ya Kahama nayo ikiwa kwenye hatua za mwisho za kuanza ujenzi wa kiwandaChato 

Hivyo Serikali ya awamu ya tano iko kazini matatizo ya wananchi kukosa soko la mifugo sasa yamefika mwisho kwani wafugaji wengi watapata masoko ya uhakika ya mifugo yao hapanchini. 

Kuhusu huduma za mifugo, Waziri Mpina alisema zoezi la uogeshaji wa mifugo ambao lilisimam akwa muda mrefu lakini kwasasa Serikali ya awamu ya tano inaogesha mifugo kila kona ya nchi na tayari wizara imegawa dawa kwenye majosho yote 1, 409 yanayo fanyakazi na kwamba wizara itaendelea kutoa dawa kwa ajili ya uogeshaji. 

Alisema wafugaji walikuwa wanateswa kuogesha ng’ombe mmoja sh 2,000 lakini sasa hivi watakuwa wanachangia gharama ndogo kwa kila ng’ombe sh 50 tu.Kuhusu operesheni za kulindarasilimali za mifugo na uvuvi, Waziri Mpina alisema wabunge wameishauri Serikali kuhusu uwekezaji wa viwanda lakini Serikali inawajibu wa kuwalinda wawekezaji wa ndani. 

“Tunazungumza uwekezaji, leo hivin ania nayeweza kuja kwenye uwekezaji kwenye nchi ambayo haiwezi kulinda rasilimali zake, na ni atakayejenga kiwanda hapa cha kusindika samaki wakati samakiwote wanatoroshwa kwenda nje ya nchi bila hata kufuatautaratibu unaokubalika ninani”alihoji Waziri Mpina, 

“Nani leo atakayekubali kuwekeza kuzalisha vifaranga, kuku, ngombe wa maziwa katika nchi ambayo maziwa yanatoka nje ya nchi hayana vibali hayajalipi wa kodi yoyote, hayajapimwa ubora na ya nauzwa na yanashindana na viwanda vya ndani nani atakayejenga viwanda hapanchini”alihoji. 

Pia Waziri Mpina alisema na nia takayejenga viwanda katika nchi ambayo inaruhusu mpaka vituv ilivyoishamuda wa matumizi kuuzwa nchini na kushindana na wazalishaji wa ndani na nia takubali. 

“lazima tukubali doria zinazoendelea zinalenga kuwalinda wazalishaji wandani ili waweze kuzalisha vizuri leo nenda kawaulize wazalishaji wa viwanda vya maziwa wa meamua kuongeza uzalishaji kwasababu kuna ulinzi madhubuti hakuna mtu ataingiza kimzahamzaha maziwa kutoka nje ya nchi”alisema Mpina. 

Aidha Waziri Mpina alisema katika vitu ambavyo alivichukia kuliko vyote miaka ya nyuma niwatukuleta vitu vilivyokwisha muda wamatumizi ambao wamepita njia za panya alafu waziri mhusika anakuja bunge ninayeye analalamika juu ya mambo hayo. 

“Wakatiyeyendioanauwezowakuwashika, sisi tutawashika na hatutakubali kuruguza wawekezaji wetu hapa nchini”alisema. Hivyo aliwaomba wabunge kuunga mkono juhudi za Serikali za kulinda rasilimali hizo kwa ajili ya manufaa ya wananchi wote kwani rasilimali hizo zikitoweka hata wao hawawezi kunufaika. 

“Nani anaye wahurumia wavuvi ni mtu ambaye anaruhusu watu wakavue kwa nyavu haramu alafu baadae mvuvi anaenda kuvua kwa gharama kubwa anarudi bila samaki au ni yule anayelinda mwisho wavuvi wa kienda kuvua wakarudi na samaki wengi ili wawe matajiri nani anayewatetea wavuvi na huo ndio msingi hasa doria hizo”alisemaMpina. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...