Na Zainab Nyamka,Globu ya Jamii
Shirikisho
la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limemtangaza mwamuzi wa mchezo wa watani
wa jadi ‘ Kariakoo Derby’ utakaopigwa kesho kwenye dimba la Uwanja wa
Taifa
Mechi hiyo inayowakutanisha mahasimu wawili kati ya Simba na Yanga utachezeshwa na mwamuzi Hance Mabena kutoka Mkoani Tanga.
TFF,
wamemtangaza Mwamuzi huyo Kijana kusimamia sheria 17 za mchezo wa soka
baada ya kuonesha uwezo mkubwa kwenye michezo yake mengine
Mabena atasaidiwa na mwamuzi mkongwe Mohamed Mkono kutoka Mkoani Tanga na kijana Kassim Mpanga kutoka Mkoa wa Dar es Salaam.
Mwamuzi wa Akiba atakuwa ni Elly Sasii kutoka Mkoa wa Dar e Salaam.
Mchezo
huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) utapigwa kesho kuanzia majira ya
saa 10 alasiri kila upande ukijinasibu kuondoka na ushindi kwenye mechi
hiyo.Yanga kinara wa TPL ana alama 58 huku watani wao Simba
wakiwa nafasi ya tatu na alama 36 akiwa amecheza mechi 15 tofauti ya
mechi zaidi ya sita na wapinzani wake
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...