16 Februari 2019

1. "Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi imefanikisha ujenzi wa kiwanda cha nyama hapa kinachoendelea kujengwa kitakuwa kinapokea Ng’ombe 50 na Mbuzi 2000 kwa siku bidhaa zote za mifugo zitatengenezwa hapa na wanufaika wa msingi ni wananchi wote, huo ni utekelezaji wa Ilani ya CCM” Ndg. Polepole

2. "Tunataka Serikali yetu ipate mapato kutokana na biashara ya mifugo na mapato hayo yawe ya haki, mapato yasiwe yana mgandamiza mfanyabishara na yatakayo kuwa rafiki kwa wafanyabishara” Ndg. Polepole

3. "Nasi kama Chama tunasema kulipa kodi hakuna mjadala lakini lazima kodi hiyo iwe inayozingatia haki” Ndg. Polepole

4. "Hapa kuna wafanyabishara wanapitisha mifugo kwenye njia za magendo na sababu  mmesema ni kodi kubwa ila wengine ni kwa sababu ya ukorofi wao tu wakuto tii sheria” Ndg. Polepole

5. "Tumezungumza na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Naibu Waziri wake na Katibu Mkuu wa Wizara  Chama kimeelekeza waje hapa Longido wazifanyie kazi changamoto zenu na ndani ya siku mbili kutoka leo Naibu Waziri atakuwa hapa” Ndg. Polepole

6. "Naye Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi atafika hapa kesho kuwasikiliza tunataka suala la usumbufu barabarani kwa wafanyabiashara wa mifugo nalo liishe, Serikali yetu ni sikivu tunaamini litakwisha” Ndg. Polepole

7. "Msimamo wetu kama Chama tozo hizi kwa wafanyabiashara wa mifugo zipungue ziwe rafiki kwa wafanyabiashara, wao wapate faida na Serikali ipate faida, wao wawe matajiri na Serikali iwe vizuri kimapato ilete maendeleo makubwa kwa wananchi” Ndg. Polepole

8. "Lengo letu kama Chama tunataka kila changamoto iliyokatika uwezo wa binaadam kutatuliwa tuitatue” Ndg. Polepole

Imetolewa na,
IDARA YA ITIKADI NA UENEZI
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...