MUIGIZAJI
maarufu nchini Steven Mengere almaarufu Steve Nyerere amemuomba radhi
msanii wa muziki wa Bongo fleva Omary Nyembo a.k.a Ommy Dimpozy.
Kwa kukumbusha
Steve Nyerere alitoa kauli ya kwamba Ommy Dimpoz hawezi tena kutoa
nyimbo yeyote kutokana na maradhi yanayomsumbua.
Hata hivyo msanii Ommy Dimpoz ameipua wimbo wake kabisa unaokwenda kwa jina la Ni wewe.Steve Nyerere baada ya Kutoka kwa wimbo huo amekuwa akishambuliwa na makundi ya watu mbalimbali mitandaoni .
Kupitia
ukurasa wake wa Istagramu Steven Nyerere leo februari 9,2019 ameandika
hivi ." kwanza nichukuwe fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu ,lakini
pili nichukuwe fursa hii kumuomba radhi ndugu yangu Dimpoz kwa namna
alivyopokea kauli yangu niliyoitoa dhidi yake na zaidi niwaombe radhi
watanzania wote na wapenzi wa Sanaa .Binadamu unapoona hapa umekosea
busara inatutaka kukiri kukosea nami nikiri kukosea kutokana na ile
kauli yangu kwa Dimpoz.
"
Lakini ifahamike kwamba kauli ile haikuwa kwamba namtakia mabaya Dimpoz
hapana ila kwa tulivyokuwa tunapata taarifa kwakweli zilikuwa
zinatukatisha tamaa," amesema Steve Nyerere.
Ameongeza
kuwa mengi yameongelewa lakini ifahamike kwamba hakuwa na nia mbaya
wala hakuwa na ugomvi na Dimpoz bali kama Binadamu hutokea kuteleza
kwenye kuzungumza na hivyo asichukuliwe kwaniambaya .
"Lakini
tunafahamu kwamba Mwenyezi Mungu hufanya miujiza yake kutokana na
sababu furani hivyo miujiza ya kumuinua ndugu yetu na kurudi kwenye kazi
zake imetokana na imani aliyonayo Dimpoz kwa muumba wake.
"
Najua mie niliteleza kwa kusema kwamba Dimpoz hatoimba tena lakini
sikuwa na nia hiyo ,kwangu natamani Dimpoz asiimbe tena Hapana kutokana
na vichekesho mbalimbali vinavyotolewa juu yangu lakini vinanifurahisha
kwani vinazidi kuupaisha wimbo mpya wa Ni wewe.
"Naomba kuchukua fursa hii kuwaomba watanzania na wapenzi wa
Muziki
kuzidi kumsapoti ndugu yetu pamoja na Kumuombea dua kwa Mwenyezi Mungu
ili azidi kuimarika kiafya."amesema Steven Nyerere.
Ikumbukwe
kuwa Ommy Dimpoz kwa muda mrefu amekuwa kimya katika muziki kutokana na
kusumbuliwa na tatizo la koo ambapo alilazimika kwenda nje ya nchi kwa
matibabu .
Hata
hivyo kwasasa afya yake imeimarika na tayari ametoa wimbo mpya wa Ni
wewe ambao umeaza kukubalika na kupendwa na wapenzi wa muziki.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...