Na Ripota Wetu,Globu ya jamii
TIMU ya wataalamu wa Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO) kwa kushirikiana na Mkandarasi ABB wa nchini Switzerland, wameendelea na kazi ya kufunga transfoma yenye uwezo wa Megawati 240 katika Kituo Kikuu cha Kupoza na Kusambaza umeme cha Ubungo jijini Dar es Salaam.
TIMU ya wataalamu wa Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO) kwa kushirikiana na Mkandarasi ABB wa nchini Switzerland, wameendelea na kazi ya kufunga transfoma yenye uwezo wa Megawati 240 katika Kituo Kikuu cha Kupoza na Kusambaza umeme cha Ubungo jijini Dar es Salaam.
Kwa
mujibu wa taarifa ya TANESCO iliyoitoa leo imesema transfoma hiyo
iliingia hapa nchini Januari 28, 2019 na lengo ni kuendelea kuboresha
hali ya upatikanaji wa umeme wa uhakika na kuleta ufanisi katika
usambazaji wa umeme katika jiji la Dar es Salaam na Pwani.
Akielezea uwezo wa Transfoma hiyo, Mkuu wa Kituo cha Kupoza na Kusambaza umeme Ubungo, Mhandisi Joseph Msumali amesema transfoma hiyo yenye uwezo wa kusukuma takribani Megawati 240 kutoka kwenye msongo wa kilovoti 220 kuelekea Msongo wa kilovoti 132 kwa ajili ya usambazaji na matumizi ya nishati ya umeme katika Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.
Akielezea uwezo wa Transfoma hiyo, Mkuu wa Kituo cha Kupoza na Kusambaza umeme Ubungo, Mhandisi Joseph Msumali amesema transfoma hiyo yenye uwezo wa kusukuma takribani Megawati 240 kutoka kwenye msongo wa kilovoti 220 kuelekea Msongo wa kilovoti 132 kwa ajili ya usambazaji na matumizi ya nishati ya umeme katika Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.
Ufungaji wa Transfoma ukiendelea
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...