UTT AMIS ni Taasisi iliyo chini ya Wizara ya Fedha ambayo inatoa huduma ya Uwekezaji kupitia mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja.

Kwa sasa inaendesha mifuko mitano ambayo ni Umoja, Wekeza Maisha, Watoto, Jikimu na Ukwasi.UTT AMIS hutoa elimu bure kwa makundi mbalimbali ili kuwawezesha kuwa na uelewa mpana juu ya masuala ya uwekezaji kwenye masoko ya fedha na mitaji.

Kwa sasa timu ya maafisa wa UTT AMIS walishiriki katika mafunzo ya wastaafu yaliyoandaliwa na Kampuni ya Taifa ya Tija ya (NIP) ili kuwajengea wastaafu watarajiwa uelewa mpana juu ya mpango wa uwekezaji kwenye mifuko inayoendeshwa na UTT.
Baadhi ya washiriki wa semina ya wastaafu iliyoandaliwa na Shirika la Tija la Taifa 'National Institute of Productivity' wakisikiliza mada juu ya uwekezaji wa pamoja pindi watakapostaafu.
Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano wa UTT AMIS, Daudi Mbaga, akitoa mada katika semina iliyoandaliwa kwa ajili ya wastaafu mkoani Morogoro iliyoandaliwa na Shirika la Tija la Taifa 'National Institute of Productivity'. 
Ofisa Masoko na Uhusiano Mwandamizi wa UTT AMIS, Martha Mashiku, akisikiliza maswali kutoka kwa washiriki wa semina.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...