Baadhi ya Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali Jijini Arusha wakifuatili kwa makini kongamano hilo lililowakutanisha kwa pamoja katika Ofisi ya Halmashauri ya wilaya ya Arusha
Mafunzo yakiendele juu ya maswala ya Afya ya uzazi chini ya vijana wenye umri wa miaka 18,ndoa xa utotoni, na mimba za utotoni.



Na. Vero Ignatus Arusha

Vyombo vya habari nchini vimetakiwa kutumia ujuzi na weredi katika kuelimisha jamii juu ya elimu ya uzazi kwa vijana chini ya umri miaka kumi na nane pamoja na kupinga vita ndoa za utotoni hali ambayo inapelekea vijana wengi kuacha kuendelea na masomo yao.

Akizungumza katika kongamano lililowakutanisha waandishi habari wa vyombo tofauti mkoani Arusha katika ofisi za halmashauri ya wilaya ya Arusha Muuguzi mkuu wa mkoa Bi Getrude Anderson amesema lengo la kongamano hilo ili kuwapa elimu wandishi wa habari juu ya maswala ya afya ya uzazi ili waweze kutumia elimu hiyo katika kuwahabarisha jamii athari za mimba za utotoni, ndoa za utotoni pamoja na elimu ya uzazi wa mpango.

Aidha Bi Getrude amesema kupitia kongamano hilo waandishi wanauwezo mkubwa wa kutumia weledi na ujuzi walionao katika kuihabarisha jamii habari za afya zenye uhakika kwani elimu huwafikia walengwaa kwa kutumia vyombo vya habari.

“Tumeamua kuandaa kongamano hili kwa kuwaaitisha waandishi habari ili kuwapa elimu waandi hawa wa vyombo mbali mbali juu ya maswala ya uzazi kwa vijana kwani waandishi hawa wakianda vipindi mbali mbali vya elimu ya uzazi vijana wataelewa mambo ya wahusuyo lakini sio hivyo tu hawawezi kuanda habari zenye weledi bila kupata ujuzi kutoka kwetu sisi wataalam wa afya,tumewataka pia waanandae makundi mbali mbali ya waandishi wa habari mbali n kuwahabarisha pia wawafuate hukuo huko vijana wawape elimu” Alisema

Alisema kupitia waandishi watapata mafanikio ya kuwafikia jamii na vijana kwani vijana wengi hufutilia sana mitandao ya kijamii ya kijamii,na hufuatilia habari hivyo wanamategemeo kupitia kongamano hilo lililofanyika italeta mafanikio mazuri sambamba kuwashauri vijana kutengeneza vikundi,na vipindi mbalimbali vya ili kufikisha elimu kwa walengwa

Alisema siku ya leo 17 februari 2019 wameaandaa tamasha ambalo litawakutanisha vijana mbali mbali mkoani arusha ambapo Tamasha hilo lita fanyika katika viwanja vya kumbu kumbu la azimio la Arusha katika mnara wa Mwenge ambapo kutakuwa nafursa za upimaji wa afya kama vile upimaji wa saratani ya shingo ya kizazi,virusi vya ukimwi na magonjwa mengineyo.,

Nae Mratibu wa mradi wa tupange pamoja Bwana Waziri Njau amesema lengo la kuwakutanisha waandishi habari ni kwa ajili ya kumtanisha kijana kwa kuandaa klabu mbalimbali na wameamua kuandaa matamasha ya vijana kupitia wandi habari ili kuwapa habari zenye weledi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...