NAIBU Waziri wa Tamisemi Mwita Waitara akizungumza na viongozi wa wilaya ya Pangani wakati wa ziara yake ya siku moja kulia ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah kushoto ni Katibu tawala wa wilaya ya Pangani Mwalimu Hassani Nyange 
Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah akizungumza wakati wa ziara hiyo kulia ni Naibu wWaziri wa Tamisemi Mwita Waitara kushoto ni Mwenyekiti wa Hlamashauri ya Pangani 
Katibu Tawala wa wilaya ya Pangani Mwalimu Hassani Nyange akizungumza wakati wa ziara hiyo 
Afisa Elimu Mkoa wa Tanga Mayansa Hashim akizungumza katika ziara hiyo 
Afisa Tawala wa wilaya ya Pangani Gibson George akisisitiza jambo wakati wa ziara hiyo 
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Pangani Mbenje Isaya akifafanua jambo wakati wa ziara hiyo 
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Pangani akizungumza wakati wa ziara hiyo kulia ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah kushoto ni Afisa Elimu Mkoa wa Tanga Mayansa Hashim 
NAIBU Waziri wa Tamisemi Mwita Waitara kushoto akisalimia na Afisa Tawala wa wilaya ya Pangani Gibson George mara baada ya kuwasili wilayani humo kwa ziara ya siku moja
NAIBU Waziri wa Tamisemi Mwita Waitara katika akiwa na Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah kushoto na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Pangani Hamisi Mnegero wakiwa kwenye kivuko cha Mto Pangani kuelekea ng'ambo ya pili ya mji huo wakati wa ziara yake
NAIBU Waziri wa Tamisemi Mwita Waitara katika akiwa na viongozi mbalimbali wakitoka kwenye kivuko cha Mto Pangani wakati wa ziara yake 
NAIBU Waziri wa Tamisemi Mwita Waitara akizungumza na wanafunzi wa shule ya Msingi Kilimangwidu wilayani Pangani wakati wa ziara yake 
Jengo linalojengwa kwenye shule ya Msingi Kilimanwidu wilayani Pangani ambalo Naibu Waziri huyo alitoa muda wa wiki tatu liwe limekamilika
NAIBU Waziri wa Tamisemi Mwita Waitara akilikagua jengo la shule ya Msingi Kilimangwidu wilayani Pangani katikati ni Katibu Tawala wa wilaya ya Pangani Mwalimu Hassani Nyange kulia ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah 
NAIBU Waziri wa Tamisemi Mwita Waitara akikagua madaftari ya wanafunzi wa shule ya Msingi Kilimangwido
Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Kilimangwido wilayani Pangani mkoani Tanga Sufiani Ramadhani katikati akitoa maelezo kwa NAIBU Waziri wa Tamisemi Mwita Waitara kushoto 



NAIBU Waziri wa Tamisemi Mwita Waitara atoa muda wa wiki tatu kwa Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Kilimangwido wilayani Pangani mkoani Tanga Sufiani Ramadhani kuhakikisha jengo linalojengwa kwenye shule hiyo linakamilika la sivyo cheo chake atakuwa amekiweka rehani.

Waitara alitoa wito huo wakati wa ziara yake wilayani Pangani iliyoambatana na kuzungumza na watumishi wa Halmashauri na kutembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa kwenye shule za msingi na sekondari wilayani humo.

Akiwa kwenye shule hiyo alizungumza na wanafunzi na baadae kutembelea Jengo ambalo linajengwa shuleni hapo ambalo ujenzi wake umechukua muda mrefu ndipo alipoonyeshwa kutokuridhishwa nalo na baadae kuamua kutoa maamuzi hayo kutokana na darasa hilo moja kujengwa kwa kipindi cha miezi sita lakini halijakamilika.

Naibu Waziri huyo alihoji kwanini jengo hilo ambalo lilipaswa kukamilika mwezi Mei mwaka 2018 lakini mpaka sasa bado halijakamilika na kueleza kwamba umefanyika uzembe mkubwa huku akimuonya Mkuu huyo wa shule kutokurudia vitendo vya namna hiyo kwa wakati mengine.

“Ni jambo la kushangaza sana tokea mwaka jana fedha zipo kwenye akaunti eti mnasubiri mfumo ufunguke hii sio sawa kabisa hata usafi mwalimu haufanyi leo ni February 11 kwa sababu hiyo nawapa wiki tatu mnatakiwa muwe mmelimaliza jengo la shule hili “Alisema

Hata hivyo Naibu Waziri huyo alimtaka Afisa Elimu Msingi wa wilaya hiyo Mwalimui Mbwana Mohamed kuhakikisha wanasimamia vyema miradi ya elimu badala ya kukaa ofisini ili kuweza kubaini changamoto zilizopo na kuona namna ya kuzipatia ufumbuzi kwa pamoja.
“Lakini pia sipendi viongozi wanapokuja ndio wanaelezwa matatizo mfumo mfumo mpo kwenye ngazi ya wilaya kusaidia viongozi wa chini mnaweze kwenda kwa Meneja wa hiyo benki mkalifanyia kazi…huu ni uzembe mkubwa umefanywa wa kutokulimaza jengo hilo kwa wakati wa sababu mna ela yakumalizi na mlipokuwa nayo tokea mwaka jana mwezi machi lakini hamjafanya hivyo,nataka ubadilike vyenginevyo cheo chao hutakuwa huna sababu ya kuendelea kuwepo kwenye nafasi yakeo “Alisema.

Awali akizunggumza Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Sufiani Ramadhanalimueleza Naibu Waziri huyo kwamba baada kupokea fedha hizo maelekezo ajenge msingi atengeneza jamvi apandishe ukuta aezeke na kupanua na kuweka mlango darasa lakini changamoto kubwa waliokumbana nayo ni
mfumo wa kibenki.Alimueleza Naibu Waziri huyo darasa hilo halijakamilika kwa sababu kwenye mfumo kuna tatizo ela hamna lakini benki zipo hivyo wakawawanashindwa kufanya matumizi.

Naya kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Pangani Mbenje Isaya alimueleza Naibu Waziri huyo baada ya kufika alijaribu kufuatilia hilo suala akagundua kuna tatizo la wao kuingiza lakini wameendele kutumia fedha zilizopo kwenye vifungu vyengine wametumia zaidi ya milioni 12
kwenye jengo hilo.

Alisema alichowaambia kwamba wahakikisha vile vifungu zitumike ili laki saba itumike kwenye kazi iliyobaki lakini pia wanachangamoto za kwao zilizopelekea kazi hiyo kuchelewa hivyo ni bora wakaziweka wazi kwako ili uweze kuzitambua.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...