Na Mwandishi Wetu, Arusha
WANARIADHA watakaoshiriki mashindano ya mbio za Nyika za
Taifa Februari 16, mwaka huu katika viwanja vya Magereza Moshi, mkoani Kilimanjaro
wameahidi kufanya makubwa zaidi.
Kufanya vizuri kwenye mashindano hayo kutawapa fursa ya kushiriki
mashindano ya mbio za Nyika za Dunia zinazotarajiwa kufanyika nchini Denmark Machi
30, mwaka huu. Wakizungumza kwenye mazoezi yaliyofanyika viwanja vya
Magereza Arusha wanariadha hao walisema chini ya mdhamini wao Mamlaka ya
Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA),wamejaa tumaini la kufanya vizuri zaidi.
Mwanariadha kutoka timu ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Anjelina
Daniel aliwashukuru NCAA kwa kuwadhamini ambapo amekuwa na wakati mzuri zaidi wa
kufanya mazoezi. “Ninawaahidi mashindano ya Nyika Moshi nitashika namba ya
kwanza hapa nimekuwa wa pili,” alisema Anjelina.
Kaimu Meneja wa Uhusiano NCAA Joyce Mgaya alisema Mamlaka
ya Ngorongoro ilitambua fursa ya uzalendo kwenye mchezo huo na mingine.“Hili ni jukwaa linaloweza kutangaza vivutio vya
utalii. Tuliona vizuri kuungana na RT kuwatia moyo wachezaji, tunaamini
watakuwa mabalozi wazuri wa utalii,” alisema Mgaya.
Naye Katibu Mkuu wa RT Wilhelm Gidabuday aliwashukuru NCAA
kwa kuwashika na mkono.
|
Kaimu
Meneja wa Mahusiano wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCCA),
Joyce Mgaya akizungumza na wanariadha kutoka Kanda ya Kaskazini viwanja
vya Magereza mjini Arusha yalipofanyika matayarisho ya kushiriki mbio
za Nyika za Taifa mjini Moshi, NCAA wamelifadhili shirikisho hilo
|








Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...