WAZIRI wa Mambo ya Ndani Mhe. Kangi Alphaxard Lugola(MB akishikana mkono na Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro wakiwa pamoja na baadhi ya viongozi wa wilaya na Mkoa wa Arusha
Mkuu wa wilaya ya Arumeru JerryMuro akionyesha moja ya gari la Polisi aina Land Rover Defender, alililifanyia ukarabati wilayani hapo mara tu alipoanza kazi mwaka jana 2018


Na. Vero Ignatus, Arusha

WAZIRI wa Mambo ya Ndani Mhe. Kangi Lugola(MB) amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry C. Muro, kwa juhudi alizozifanya za Kukarabati Gari ya Polisi aina Land Rover Defender, ambalo lilikuwa halitumiki kwa miaka mingi kutokana na kuchakaa na kuwa chuma chakavu, ambapo ukarabati huo umegharimu zaidi ya Tshs. Milioni 19. 

Mhe. Kangi Alphaxard Lugola amesema juhudi zilizofanywa na Mhe. Jerry C. Muro, kuwezesha ukarabati wa Gari hiyo ambayo imekarabitiwa na wadau wa maendeleo wa Wilaya ya Arumeru, kutasaidia kuimarisha Ulinzi katika maeneo ya Mamlaka ya Mji Mdogo wa Ngaramtoni. 

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry C. Muro, amesema Kwa kipindi cha miezi mitano alichotumikia wananchi wa Arumeru, amemua kutatua changamoto za vifaa vya kutendea kazi Kwa jeshi la Polisi ikiwemo kukarabati Magari yote ya Jeshi la Polisi Wilaya ya Arumeru, kwa kuwashirikisha wadau, badala ya kusubiria fedha kutoka Serikali Kuu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. https://youtu.be/j6a0tF8QnKk

    ReplyDelete
  2. Kansa ya matiti dalili zake
    https://youtu.be/j6a0tF8QnKk

    ReplyDelete
  3. KANSA YA MATITI DALILI ZAKE
    https://youtu.be/j6a0tF8QnKk

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...