WAZIRI wa Mambo ya Ndani Mhe. Kangi Alphaxard Lugola(MB akishikana mkono na Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro wakiwa pamoja na baadhi ya viongozi wa wilaya na Mkoa wa Arusha
Mkuu wa wilaya ya Arumeru JerryMuro akionyesha moja ya gari la Polisi aina Land Rover Defender, alililifanyia ukarabati wilayani hapo mara tu alipoanza kazi mwaka jana 2018
Na. Vero Ignatus, Arusha
WAZIRI wa Mambo ya Ndani Mhe. Kangi Lugola(MB) amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry C. Muro, kwa juhudi alizozifanya za Kukarabati Gari ya Polisi aina Land Rover Defender, ambalo lilikuwa halitumiki kwa miaka mingi kutokana na kuchakaa na kuwa chuma chakavu, ambapo ukarabati huo umegharimu zaidi ya Tshs. Milioni 19.
Mhe. Kangi Alphaxard Lugola amesema juhudi zilizofanywa na Mhe. Jerry C. Muro, kuwezesha ukarabati wa Gari hiyo ambayo imekarabitiwa na wadau wa maendeleo wa Wilaya ya Arumeru, kutasaidia kuimarisha Ulinzi katika maeneo ya Mamlaka ya Mji Mdogo wa Ngaramtoni.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry C. Muro, amesema Kwa kipindi cha miezi mitano alichotumikia wananchi wa Arumeru, amemua kutatua changamoto za vifaa vya kutendea kazi Kwa jeshi la Polisi ikiwemo kukarabati Magari yote ya Jeshi la Polisi Wilaya ya Arumeru, kwa kuwashirikisha wadau, badala ya kusubiria fedha kutoka Serikali Kuu.
https://youtu.be/j6a0tF8QnKk
ReplyDeleteKansa ya matiti dalili zake
ReplyDeletehttps://youtu.be/j6a0tF8QnKk
KANSA YA MATITI DALILI ZAKE
ReplyDeletehttps://youtu.be/j6a0tF8QnKk