Diwani wa kata ya Tengelea Shabani Manda wa (pili kushoto) akimkabidhi Katibu wa Jumuiya ya Wazazi wa (CCM) Mkoa wa Pwani,Gama J Gama baiskeli kwa watu wenye ulemavu wa miguu katika kongamano la elimu lililofanyika shule ya msingi Hoyoyo wilaya ya mkuranga mkoa wa Pwani.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi wa (CCM) Mkoa wa Pwani,Gama J Gama akiukabidhi Slyveter Bedu cheti cha taaluma katika katika kongamano la elimu lililofanyika katika shule ya msingi Hoyoyo wilaya ya mkuranga mkoa wa Pwani.(Picha na Emmanuel Massaka,MMG)
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi wa (CCM) Mkoa wa Pwani,Gama J Gama (kulia) akikabidhi tanki la maji lita 2000 uongozi wa shule ya msingi hoyoyo iliyopo kata ya Tengelea wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani.
Diwani wa kata ya Tengelea Shabani Manda akizungumza na wazani pamoja na wale katika kongamano la elimu lililofanyika katika shule ya msingi Hoyoyo wilaya ya mkuranga mkoa wa Pwani Alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wazazi kuwekeza kwenye elimu kwa watoto kwani huo ndiyo urithi wenye thamani katika maisha yao.
Katibu wa Mbunge,Omar Kisatu akiwasisitiza wanafunzi wa shule ya msingi hoyoyo iliyopo kata ya Tengelea wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani. kusoma kwa bidii ili malengo yao yatimie.
Katibu wa CCM Kata ya Tengelea Twahiri Koki akizungumza na wazazi na walezi katika kongamano la elimu lililofanyika katika shule ya msingi Hoyoyo wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani ambapo aliwaomba waache tamaduni za zamani wapeke watoto shule watawasaidia baadae wazazi hao.
Picha ya pamoja


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...