UTALII WETU ARUMERU 

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Muro ameanzisha mkakati Maalum wa kukuza utalii katika Hifadhi ya wanyama ya Arusha iliyoko wilaya ya Arumeru kwa kuvitumia Vyuo vikuu na taasisi za Elimu ya Juu , Shule za sekondari binafsi na za Umma pamoja na shule za msingi na za awali zilizoko katika wilaya ya Arumeru .

Dc Muro amebuni mkakati huo ikiwa ni mwendelezo wa kampeni yake ya kuhamasisha utalii wa ndani katika wilaya ya Arumeru ambapo safari hii ametoa maelekezo kwa wamiliki , viongozi , wakuu wa vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu pamoja na wakuu wa shule kuweka utaratibu utakaowawezesha wanafunzi na jumuiya za watu walio kwenye taasisi zao kutembelea hifadhi ya Wanyama Arusha.

Aidha kwa kuanzia mara mbili kwa mwaka, ambapo katika zoezi la mwanzo Dc Muro amewaongoza wanafunzi , walimu na wanajumuiya ya Shule ya Haradali Winners kutembelea hifadhi ya wanyama ya Arusha ambapo miongoni mwao ni wanafunzi walioapata alama ya ufaulu ya daraja la kwanza (division one ) kutoka kila darasa na mikondo ya shule hiyo kwa gharama za Dc Muro, ambapo mwezi ujao atapeleka kundi lingine la wananfunzi wa shule ya sekondari ya Ilboru iliyoko Halmashauri ya Arusha wilaya ya Arumeru .
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Muro akiwa na baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Haradali Winners ambao emeongozana nao kutembelea hifadhi ya wanyama ya Arusha,wakisoma maelezo kwenye vitabu vya utalii kuhusu hifadhi hiyo




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...