Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 7 la Afya na Sayansi la Afrika Mashariki lililofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasha mwenge kama ishara ya ufunguzi wa Kongamano la 7 la Afya na Sayansi la Afrika Mashariki lililofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Sehemu ya Wataalamu waliohudhuria ufunguzi wa Kongamano la 7 la Afya na Sayansi la Afrika Mashariki lililofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
amesema teknolojia ni zana muhimu katika kushughulikia mapungufu ya
msingi katika sekta ya afya.
Makamu wa Rais ameyasema hayo leo wakati wa Ufunguzi wa Kongamano la 7 la Afya na Sayansi la Afrika Mashariki lililofanyika kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.“tunahitaji kuwekeza katika teknolojia ya afya ya kidijitali kama njia ya kuboresha na kuimarisha huduma ya afya za kikanda” alisema Makamu wa Rais.
Makamu wa Rais ametanabaisha kuwa Tanzania imeweza kutambua na kuanza kujenga mfumo wetu wa huduma za afya kupitia Wizara ya Afya na mashirika kadhaa kama vile MSD (ambayo teknolojia ya kidijitali inasaidia kufuatilia usambazaji kutoka hatua ya ununuzi hadi utoaji kwa uhakika), NHIF (usimamizi wa uanachama wa mteja, kudai na mchango) na TFDA (taarifa ya mtandaoni ya kuagiza na kuuza nje chini ya TFDA na taarifa ya mtandaoni ya madhara mabaya ya matumizi ya dawa na vipodozi) pia kuna Mfumo wa Usimamizi wa Hospitali haswa katika Hospitali zote za Serikali. Mfumo huu hutoa taarifa halisi ya muda na unaweza kufuatilia harakati za mgonjwa na za dawa.
Mkutano huo unaofanyika kila baada ya miaka miwili unawakusanyisha wadau wa sekta za afya kutoka Afrika Mashariki na Wataalamu kutoka sehemu mbalimbali duniani ambao una lengo la kuangalia namna ya kutumia utaalamu wa kisasa katika huduma ya afya kwa kutumia mfumo wa kidijitali.
Kwa upande wake Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema Kongamano hili linafanyika wakati ambapo kanda hii, na Afrika nzima, inahitaji mabadiliko ya teknolojia ya haraka hasa katika teknolojia ya kidijitali ili kusaidia utekelezaji wa hatua za sekta za afya na mipango na kuongeza kasi ya kufikia Ufikiaji wa Afya wa Ulimwengu (UHC) ili kufikia kufikia Lengo la Maendeleo Endelevu (SDG) 3 kwa ujumla.
Wakati huohuo Makamu wa Rais amekutana na kufanya mazungumzo na Binti wa Mfalme wa Jordan Sarah Zeid ambapo walizungumzia masuala mbali mbali ya kuboresha lishe na afya kwa Mama na Mtoto.
Binti huyo wa Mfalme aliambata na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Mpango wa Chakula Duniani Bw. Michael Dunford.
Makamu wa Rais ameyasema hayo leo wakati wa Ufunguzi wa Kongamano la 7 la Afya na Sayansi la Afrika Mashariki lililofanyika kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.“tunahitaji kuwekeza katika teknolojia ya afya ya kidijitali kama njia ya kuboresha na kuimarisha huduma ya afya za kikanda” alisema Makamu wa Rais.
Makamu wa Rais ametanabaisha kuwa Tanzania imeweza kutambua na kuanza kujenga mfumo wetu wa huduma za afya kupitia Wizara ya Afya na mashirika kadhaa kama vile MSD (ambayo teknolojia ya kidijitali inasaidia kufuatilia usambazaji kutoka hatua ya ununuzi hadi utoaji kwa uhakika), NHIF (usimamizi wa uanachama wa mteja, kudai na mchango) na TFDA (taarifa ya mtandaoni ya kuagiza na kuuza nje chini ya TFDA na taarifa ya mtandaoni ya madhara mabaya ya matumizi ya dawa na vipodozi) pia kuna Mfumo wa Usimamizi wa Hospitali haswa katika Hospitali zote za Serikali. Mfumo huu hutoa taarifa halisi ya muda na unaweza kufuatilia harakati za mgonjwa na za dawa.
Mkutano huo unaofanyika kila baada ya miaka miwili unawakusanyisha wadau wa sekta za afya kutoka Afrika Mashariki na Wataalamu kutoka sehemu mbalimbali duniani ambao una lengo la kuangalia namna ya kutumia utaalamu wa kisasa katika huduma ya afya kwa kutumia mfumo wa kidijitali.
Kwa upande wake Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema Kongamano hili linafanyika wakati ambapo kanda hii, na Afrika nzima, inahitaji mabadiliko ya teknolojia ya haraka hasa katika teknolojia ya kidijitali ili kusaidia utekelezaji wa hatua za sekta za afya na mipango na kuongeza kasi ya kufikia Ufikiaji wa Afya wa Ulimwengu (UHC) ili kufikia kufikia Lengo la Maendeleo Endelevu (SDG) 3 kwa ujumla.
Wakati huohuo Makamu wa Rais amekutana na kufanya mazungumzo na Binti wa Mfalme wa Jordan Sarah Zeid ambapo walizungumzia masuala mbali mbali ya kuboresha lishe na afya kwa Mama na Mtoto.
Binti huyo wa Mfalme aliambata na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Mpango wa Chakula Duniani Bw. Michael Dunford.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...