Mama wa mitindo Asya Idarous Khamsin  Jumamosi hii ya Machi 9, ataingia na  Wanawake wa Tanzania kusherehekea siku ya Wanawake Duniani kwa kuonesha Mitindo yake katika jukwaa hilo maalum litakalo wakutanisha pia wabunifu mbalimbali. 

Hii itakuwa ni fursa ya kipekee kwa watu mbalimbali watakaojitokeza kushuhudia Mama wa mitindo ambaye kwa muda mrefu amekuwa akishiriki kuonesha mitindo yake nchini Marekani pamoja na mataifa ya Ulaya. 

"Mitindo mipya ya Ubunifu ya mavazi nitaonesha katila katika jukwaa la Tanzanite Women's hapa Dar.  Lakini pia tutauza karibuni sana" alieleza Mama wa mitindo Asya Idarous Khamsin  

Tanzanite Women's Forum & Runch ni jukwaa kubwa la Wanawake ambapo ufanyika kila mwaka huku Wanawake wenye ushawishi wakipata nafasi ya kuzungumza katika nyanja mbalimbali za kufikia malengo ya kibishara.

Tukio hilo linatarajia kufanyika katika ukumbi wa Double tree by Hilton hotel Masaki Jijini Dar Es salaam.

Wabunifu wengine mbali na Mama wa Mitindo Asya Idarous,  ni pamoja na Mustafa Hassanali, Vivya shaa, Abdul Mwene,Mgeci Cici, Zamda George.

Wabunifu wengine ni Irada Style, Katty Collection, Malika  Designer. 

Aidha, watoa mada na wazungumzaji wakuu kwenye tukio hilo ni pamoja na Mwanahamisi Singano, Smart Money Decisions  na Lavie Makeup artist. 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...