Habari na Picha na 
Dixon Busagaga, Moshi
MVUA kubwa iliyoambatana na upepo imesababisha adha kwa watumiaji wa BARABARA kadhaa katika mji wa Moshi baada ya miti kukatika na kufunga barabara.
Globu ya Jamii  imepita maeneo kadhaa ya mji wa Moshi na kujionea kadhia hiyo huku maeneo mengine wananchi wakijitolea kuondosha miti iloyoanguka barabarani kwa kuikata huku watumiaji wa vyombo vya moto wakilazimika kunadili njia za kupita .
Maeneo ambayo watumiaji wa vyombo vya moto wameathirika ni pamoja  barabara ya Shanty town,barabara ya International school pamoja na barabara ya Shule ya sekondari Mawenzi.
Maeneo mengine imeshuhudiwa miundombinu ya umeme ikiwa imeharibika baada ya nguzo kukatika na nyaya kuangakua katikati ya barabara.










Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...