Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akifafanua jambo katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, kilichofanyika Bungeni, jijini Dodoma leo. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali, Jacob Kingu. Kulia ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Phaustine Kasike.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (katikati) akifurahia jambo wakati alipokua anazungumza na Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Victor Mwambalaswa, na Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini, Prosper Mbena, wakati walipokua wanatoka katika kikao cha Kamati hiyo, kilichofanyika Bungeni, jijini Dodoma leo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Mussa Zungu (kushoto meza kuu), akiwa na wajumbe wa kamati hiyo, wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (hayupo pichani) alipokua akifafanua jambo katika kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika Bungeni, jijini Dodoma leo. Waziri Lugola aliambatana na Watendaji Wakuu wa Wizara yake katika kikao hicho.
Naibu Katibu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ramadhani Kailima (kushoto) akifurahia jambo na Mbunge wa Viti Maalum, Amina Mollel, mara baada ya Naibu Katibu Mkuu huyo kutoka katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, kilichofanyika Bungeni, jijini Dodoma leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...