Kuanzia siku ya Jumatatu, tarehe 1 mwezi Aprili,wasikilizaji wa vipindi vya Kiswahili vya BBC watasikiliza ladha mpya  ya vipindi vya Dira ya Dunia na Amka na BBC.Mabadiliko haya yatahusisha pia watangazaji wapya na kutambulishwa kwa habari bora kuhusu biashara pamoja na Makala zenye kuleta matokeo chanya.

Matangazo ya barabarani yatafanyika Kenya na Tanzania katika uzinduzi huu.Matangazo hayo yatafanyika katika mji wa Bandari Mombasa, mji wa Kwale, Kitui, Dodoma,Morogoro,Kibaha na Dar es Salaam.Wasikilizaji watasikia matangazo hayo maalumu kwa kipindi cha siku tano, kutoka kwenye maeneo hayo na kusikia sauti za watu mbalimbali katika maeneo tutakayoyafikia.

 -Mahojiano na watu mashuhuri na viongozi:
- Wanamuziki - Venessa Mdee, Susumila and Mwasiti
- Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai
- Gavana wa Mombasa, Ali Hassan Joho
- Mbunge wa Tanzania, Zitto Kabwe
- Mwanasiasa wa upinzani kutoka visiwani Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamadi
- Rais mstaafu wa awamu ya pili wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi
- Mkuu wa wilaya, Jokate Mwegelo
- Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Winnie Kiiza
- Mbunge wa Tanzania na mke wa Rais wa awamu ya nne,Salma Kikwete
- Rais wa zamani wa Tanzania , Jakaya Kikwete
- Gavana wa Machakos,Dokta Alfred Mutua

Taarifa motomoto:
-‘’ Wahandisi’’ wanawake wa Zanzibar
- Wanakijiji watengeneza mkate wa wadudu
- Nyumba iliyojengwa katikati ya mpaka wan chi mbili
- Uvutaji wa sehemu za siri za wanawake nchini Rwanda
- The Kenyan community without sweat pores
-Jamii ya Kenya isiyotoa jasho
- Kisiwa chenye uhaba wa Condom

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...