Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simoni Sirro amefanya ziara katika mitaa
mbalimbali ya Kariakoo kwa lengo la kutaka kujua hali ya kiusalama
katika maeneo hayo, zaidi ikiwa kuwasikiliza wananchi wan maoni gani juu
ya ushirikiano wao na Jeshi la Polisi katika utendaji kazi wa kila
siku.
Aidha amewashukuru wananchi na wafanyabiashara wa Kariakoo kwa ushirikiano wao huku akiwataka waendelee kuwafichua wahalifu wa mifukoni na wale wanaotumia udanganyifu wa kuwaibia watu kwa kuwauzia sabuni na kusema mwisho wao hauta kuwa mzuri maana uhalifu hauna nafasi nchini.
IGP Sirro amewataka wananchi wote kwa ujumla kuendelea kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi hasa pale wanapokuwa na shaka na jambo fulani ili hatua z mapema ziweze kuchukuliwa kwa lengo la kuulinda usalama na amani iliyopo nchini, lakini pia amewahakikishia wananchi kuwa katika kipindi hiki cha sikukuu za Pasaka Jeshi la Polisi limejipanga vizuri kuhakikisha kuwa linasimamia usalama wa raia na mali zao ili waweze kusherekea wakiwa salama.
Aidha amewashukuru wananchi na wafanyabiashara wa Kariakoo kwa ushirikiano wao huku akiwataka waendelee kuwafichua wahalifu wa mifukoni na wale wanaotumia udanganyifu wa kuwaibia watu kwa kuwauzia sabuni na kusema mwisho wao hauta kuwa mzuri maana uhalifu hauna nafasi nchini.
IGP Sirro amewataka wananchi wote kwa ujumla kuendelea kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi hasa pale wanapokuwa na shaka na jambo fulani ili hatua z mapema ziweze kuchukuliwa kwa lengo la kuulinda usalama na amani iliyopo nchini, lakini pia amewahakikishia wananchi kuwa katika kipindi hiki cha sikukuu za Pasaka Jeshi la Polisi limejipanga vizuri kuhakikisha kuwa linasimamia usalama wa raia na mali zao ili waweze kusherekea wakiwa salama.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...