Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Tanga Ummy Mwalimu akizungumza wakati wa uzinduzi wa kambi ya macho kwenye shule ya Sekondari Maawal Jijini Tanga chini ya Taasisi ya Bilal Muslim Mission Tanzania wakishirikiana na Mbunge huyo chini ya Ufadhili wa better Charity ya nchini Uingereza kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa kushoto ni Mwenyekiti wa Bilal Muslim Africa Mohsin Abdallah (Shein) 
Mwenyekiti wa Bilal Muslim Africa Mohsin Abdallah (Shein) akizungumza wakati wa uzinduzi huo kulia ni Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kushoto ni Mkuu wa Maawal Sheikh Mohamed Hariri
MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akizungumza wakati wa halfa hiyo 
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Clemence Marcel akizungumza wakati wa uzinduzi huo
Mratibu w Bilal Muslim Mission of Tanzania Sharriff akizungumza wakati wa uzinduzi huo
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu katikati akiteta jambo na Mratibu wa Bilal Muslim Mission of Tanzania Sharrif mara baada ya kufanya uzinduzi huo kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu katikati akiteta jambo na mmoja wa wanafunzi ambaye alijitokeza kwenye kambi hiyo ya matibabu ya macho mara baada ya kuizindua 
Sehemu ya wananchi wakifuatilia hotuba ya Waziri Ummy wakati akizindua matibabu hayo
Wananchi kutoka maeneo 
Sehemu ya wananchi wakisubiriwa kupata huduma ya matibabu wakati wa kambi hiyo
Sehemu ya wananchi waliojitokeza kwenye kambi hiyo ya macho


MAELFU ya Wakazi wa mji wa Tanga wamejitokeza kwenye kambi ya Matibabu ya Macho inayoendelea kwenye shule ya shule ya Sekondari Maawal mjini hapa chini ya Taasisi ya Bilal Muslim Mission tanzania wakishirikiana na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto chini ya Ufadhili wa better Charity ya nchini Uingereza

Akizungumza wakati akizindua kambi hiyo ya matibabu ya Macho Waziri Ummy alisema kuwa tatizo la ugonjwa wa macho nchini limekuwa kubwa ambapo kila watanzania mia moja wanne wanakabiliwa na matatizo ya macho. Alisema takwimu hizo zimefafanua kuwa katika idadi hiyo kila mtanzania mmoja anakabiliwa na tatizo la upofu wa mamcho na watanzania watatu wanakabiliwa na matatizo ya upungufu wa uoni wa kati na hali ya juu tatizo ambalo limekuwa kubwa sana. 

Aidha alisema kwa mujibu wa takwimu wizara ya afya katika kila watanzania 100 mmoja ana tatizo la upofu huku kwa ikieleza kwa watanzania 100 kati yao watatu wana matatizo ya upungufu wa kuona wa kati na hali ya juu tatizo hilo ni kubwa kwa sababu kati ya watu 100 wa nne wana matatizo ya macho. 

Kufuatia hali hiyo Waziri Ummy alitoa wito kwa watanzania kujiwekea utaratibu wa kuhudhuria kwenye vituo vya Afya ili waweze kupata matibabu pindi wanapoona kuwepo dalili za ugonjwa wa macho. “Ukiona una tatizo la macho nenda kwenye vituo vya afya upate matibabu haraka lakini niwaambie pia wana tanga na watanzania hakikisheni mnachunguza afya ya macho na afya ya kinywa mara moja kila mwaka “Alisema .

Waziri huyo aliwataka watanzania kuzingatia ulaji wa vyakula unaofaa hasa vyenye vitamin ikiwemo kuhakikisha wanakula mbogamboga huku akiwataka kuacha dawa kwenye macho bila kuandikiwa na daktari kwa sababu inaweza kupelekea kuharibu macho yao .Awali akizungumza katika halfa hiyo Mwenyekiti wa Bilal Muslim Afrika Mohsin Abdallah (Shein) alimshukuru Rais Dkt John Magufuli kwa kuhakikisha huduma za afya nchini zinaimarika kwenye maeneo mbalimbali na kuondosha changamoto zilizopokuwepo awali.

“Namshukuru Rais Magufuli miaka yote tumefanya kazi tunatumia hospitali za serikali huduma zilikuwepo lakini hazikuwa kama ilivyo sasa lakini leo serikali ya awamu ya tano hospitali zimekuwa na vifaa muhimu kwenye hospitali”Alisema 

Aidha alisema wao kama bilal Muslim wamekuwa wakienda kwenye maeneo ambayo yana matukio makubwa lakini kutokana na ombi la Waziri Ummy tumeona kuja hapa kumuunga mkono pia tunashukuru mwamko umekuwa mkubwa sana,

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...