Mwili wa mwanamuziki mkongwe wa muziki rhumba wa nchini DR Congo, Marehemu Lutumba Simaro Masiya ukifanyiwa ibada ya kuuaga katika moja ya kanisa huki jijini Paris, Ufaransa leo, ambapo unatarajiwa kuusafirisha na ndege ya "Air France" kuelekea Kinshasa, nchini Congo kwa mazishi.

Mwili wa Marehemu Lutumba Simaro Masiya ukiwasili jijini Kinshasa, moja kwa moja utapelekwa kuhifadhiwa "Mortuary katika hospitali De Cinquantenaire, na baadaye kupewa heshima za mwisho bungeni, kabla ya kufika bungeni, atapitishwa nyumbani kweke, na kufikishwa pia kwenye "Lutumba Monument"sehemu yenye mnara wa kumbukumbu yake ili kuwapa nafasi wapenzi wa muziki wake kuuaga mwili wa mpendwa wao.

Mwili wa marehemu Lutumba Simaro Masiya utalazwa kwenye makazi yake ya milele kwenye makaburi ya "Nécropole Entre Terre et Ciel", jijini Kinshasa siku ya jumapili Aprili 29, 2019..

Marehemu Lutumba Simaro Masiya ambaye jina lake halisi ni "Apa Simon Lutumba Ndomanueno" alifariki Machi 30, 2019 jijini Paris nchini Ufaransa, akiwa na umri wa miaka 81. Atakumbukwa kwa nyimbo zake nyingi ikiwemo "Maya" (unaweza iangalia hapa chini).

Sehemu ya waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Marehemu Lutumba Simaro Masiya, walipokuwa wakitoka kanisani kulikofanyika ibada maalum ya kuaga, jijini Paris Ufaranza.
Ankal pia anamkumbuka mkongwe huyo wa Muziki wa Rhumba walipokutana jijini Kinshasa. Mungu ailaze pema peponi roho yake - Ameen

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...