Tanzania inatarajia kuwa mwenyeji wa michuano ya kimataifa ya Karate ambayo yamepangwa kuanza kurindima nchini Mwezi July jijini Dar es salaam, kwa kushirikisha mataifa ya bara la Afrika bara la Asia.

Taarifa za kufanyika kwa tukio hilo la kimataifa katika radhi ya Tanzania upande wa mchezo wa Karate, zimetolewa na Mkufunzi mkuu wa Karate tawi la Tanzania Jorome George Mhagama alipozungumza na kipindi hiki jijini Dar es salaam.

Mhagama amesema ni faraja kwa viongozi wa chama cha Karate nchini kuendelea kupata nafasi ya kuandaa michuano hiyo ya kimataifa, jambo ambalo ambaamini linaendelea kuitangaza nchi ndani ya Afrika na ulimwenguni kwa ujmla.

Mhagama amesema lengo kubwa la kufanyika kwa michuano hiyo, ni kuendelea kutoa nafasi ya kujifunza kwa wachezaji wan chi shiriki, kujenga urafiki na uhusiano ambao utaendelea kuifanya Tanzania kuwa na nafasi ya kutambulika zaidi kimataifa.

Pia ameelezea shughuli nyingine ambazo zitakwemnda sambamba na michuano hiyo ya kimataifa, ikiwa ni pamoja na kufanyika kwa semina na mitihani nadharia na vitendo.

Wakati huo huo Mhabama akaweka wazi ratiba ya matukio yote kuelekea michuano hiyo ya kimataifa pamoja na semina itakayofanyika nchini Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...