Ay,Mwanafa wadaiwa  kudhulumiwa haki zao

WASANII  wote nchini wameombwa kujitathimini upya katika mikataba au makubaliano wanayoingia na makampuni, mashirika, wamiliki wa filamu kwenye kazi zao.

Akizungumza na wasanii wakili wa wasanii Alberto Msando  katika kongamano la waigizaji lililoandaliwa na  bodi ya filamu (TFB)  pamoja na chama cha waigizaji (TDFAA)  lililofanyika ukumbi wa Suma JKT Mwenge jijini Dar es salaam. amesema ni wakati wa Wasanii kujitathimini na kuingia makubaliano ya kikazi kwa njia ya maandishi ili kuepuka unyonywaji na utapeli kwenye malipo baada ya kazi na kabla ya kazi.

"Mikataba inasaidia wasanii kuwa na adabu na nidhamu ya kazi kutokana na kumtaka muda maalum kuwepo kwenye kazi na hata hivyo inamsaidia msanii kudai stahiki zake  haraka huku akiwa na vielelezo husika ," alisema Msando.

Msando amewataja baadi ya wadau wakiwemmo waandaaji wa filamu,watunzi wa filamu pamoja na watengenezaji wa matangazo ambao wanawatumia wasanii kwenye matangazo hayo, kuwa na leseni za kikazi ili kutambulika kisheria.

Halikadhalika amewatolea mfano wasanii kama Ambwene Yesya a.ka AY Khamisi Mwinjuma a.k.a MwanaFA,Wema Sepetu pamoja na Masanja Mkandamizaji ambao wameshapata matatizo kwenye kazi zao kutokana na mikataba wanayoingia na wakifika katika mikono sheria wanafanikiwa kupata haki zao ,Hivyo amewasihi wasanii kufika kwenye vyombo vya sheria au hata kusaini mikataba na kuhusisha Mawakili .

Pia ametoa rai kwa wasanii kujiandikisha kwenye vyama vya sanaa,bodi ya filamu pamoja baraza la sanaa ili kutambulika kama msanii mwenye kutambulika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...