MJASIRIAMALI Devotha David ambaye ni mmiliki wa First Supper Market iliyopo mbezi Mbeach kona ya Goba Dar es Salaam amefurahia kupewa tuzo ya mafanikio makubwa ya Thamani ya Mwanamke na ajira binafsi siku chache zilizopita Jijini Dar es Salaam. 

Kongamano hilo lenye mafanikio makubwa lilianza kuandaliwa mwaka 2017 limekuwa la malengo mazuri kwa kutambua kazi za jamii kwa wanawake. “Kwa mara hii nafurahia kufanikiwa kwangu ikiwa nimeweza kutambulika kama mwanamwake niliyejiajiri na Kusherekea Siku hii,”anasema Devota. 

Alisema nashukuru kupata tuzo yenye lengo la kuipa thamani Ajira binafsi sawa na Ajira rasmi ambayo inachukua kiasi kidogo cha wanawake kulinganisha na ajira binafsi. Aidha alisema kuwa amefanikiwa kukutanishwa katika jukwaa hilo la wanawake wanawake zaidi, na ameweza kujengewa ujasiri wa kuendeleza mapambano ya mafanikio kupitia jukwaa hilo na sasa ataweza kufanikiwa zaidi kwani maadhimio ya mafanikio yake hayo atayazidisha kwa bidii ili kuzidi kung’ara baada ya kongamano hilo . 

Amewaomba waandaaji kuendelea kufanya vizuri tena Kongamano hilo kwani kutakuwa na mafanikio makubwa yaliogusa maisha ya wanawake wa Tanzania. “Nawaomba wanawake wenzangu waliojiajiri kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kufanya maandalizi ya kukutana na wanawake wengine Siku nyingine tena ambapo hisstoria itajiandika tena,”alisema Devotha. Alisema kuwa ameweza kuendesha biashara zake kwa muda mrefu na kupata mafanikio makubwa zaidi anajivunia kupata msaada zaidi kutoka kwa mumewe.

“Nikiwa katika mazingira ya utoto zamani nilianza kuwa namsimamia mama yangu mzazi kipindi nikitoka shule niliachiwa biashara na mama , mama alikuwa akimili depo moja niliweza,”alisema Devotha. Alisema hivyo kutokana na kuanza mapema mazingira hayo aliyokuwa , alianza kupenda ajira za kujiajiri, ambapo kwa sasa taswira ya serikali ya awamu ya tano inapigania vipao mbele katika ajira za wajasiriamali binafsi. 

Kwa taswira ya ajira kwa serikari zinapambanuliwa kuwa ajira zinaweza kuwa moja kwa moja kutoka serikalini au kuweka mazingira ya kuziwezesha sekta binafsi kutekeleza jukumu yake. Hata hivyo kumekuwa na hatua za wanawake kupambaniwa , Siku ya wanawake Duniani ambayo uadhimishwa kila mwaka ifikapo Tarehe 8 Mwezi wa Tatu Kimataifa; kumekuwa na umuhimu mkubwa wa kuutambua mchango wa wanawake katika nyanja Mbalimbali na kumuinua mwanamke azidi kusimama na kuinuka kimaendeleo katika Jamii ulimwenguni. Lengo kuu la kuadhimisha siku hiyo adhimu ni kutathmini utekelezaji wa afua za kufikia usawa jinsi na uwezeshaji wanawake kiuchumi, kijamii,kisiasa katika kufikia maendeleo jumuishi. 

Maadhimisho haya, pia yanatoa fursa ya kuelimisha jamii kuhusu jitihada mbalimbali zilizofanywa na jamii, serikali, asasi za kiraia, sekta binafsi na wadau wa maendeleo katika kumwinua mwanamke. Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Samia Suluhu kupitia kaulimbiu ya ‘kuelekea Uchumi wa Viwanda: Tuimarishe Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji wa Wanawake Vijijini’. Anasema kuwa amekuwa akiwataka wanawake kutambua kuwa serikali imekuwa ikiwahudumia, kuwathamini, kuwawezesha na kuwasimamia vyema ili kuhakikisha usawa wa kijinsia unakuwepo katika jamii. Devotha alisema kuwa juhudi hizo za serikali ni za ukweli zipo zinaelekeza juu ya kuweleka mafanikio bora kwa mwanamke . 

Licha ya kuziunga mkono juhudi hizo anaelezea heka keha zake kuelekea ukombozi zaidi juu yake katika anga za uchumi katika familia yake. Harakati za nyumani kwao kupitia mama yake mzazi bado zinaonekana kumjenga katika itaji lake la kuutaka msingi bora wa kufikia malengo makubwa ,anaeleza kuwa anayo jumla maduka matatu katika jiji la Dar es Salaam . 

“Najishughulisha na maduka yangu yanayouza bidhaa mbali mbali kama mabegi ya watoto viatu vya watoto pamoja na mambo mengine kama hayo ya mavazi ya aina yote kwa umri huo ,”alisema. Amesema First Supper Market iliyopo mbezi Mbeach kona ya Goba Dar es Salaam ni moja ya mafanikio yake mapya kwa sasa. 

Alisema kuwa kwa kufungua saloon yake ya kike hapa jijini, kila jambo huwa na safari yake kimafanikio, mtaji wa saloni ndio uliokuwa mtaji wake wa kwanza katika maisha yake . “Baada ya kuhapo nilifanikiwa kuanza biashara ya kwenda nje kununua mavazi ya biashara taratibu nilianza kupata uzoefu na hatimaye niliweza kumudu napo ikiwa moja ya mafanikio niliyo nayo,”alisema. Amesema kuwa angependa kuona furaha yake ikizidi kukua na kupata tabasamu lenye furaha kama ilivyo kwa mafanikio kutoa faraja ya kweli katika maisha. 

“Niliwahi pia kumiliki mtaji mkubwa wa kuendesha baa iliyokuwa na vyumba vya kulala wageni kupitia mradi huo niliweza kupata pesa nyingi lakini iliweza kunifanya niwe mbali na familia ,”alisema. Devota anaeleza kuwa mara baada ya kuendesha kwa mafanikio mradi wake wa Dipromatic Baa iliyokuepo maeneo ya tabata jijini hapa kimsingi ndio iliyo ujenga mtaji wake kuwa mkubwa katika biashara , Dipromatic iliweza kujizolea umaarufu mkubwa ,iliweza kuwa na wateja wengi alikuwa mbali na famili muda wa kukaa nyumbani ulikuwa mchache. 

Amesema kuwa Dipromatic Baa aliendesha kwa miaka kadhaa na ndiyo chachu ya mafanikio, na ndpo alipoaanzia mradi alionao sasa wa biashara nyingine alizonazo kwa sasa ambapo bahari Beach anaduka pamoja na Min Supper Market zote zikiwa na jina hilo la First Supermarket. 

Amesema kuwa anawakaribisha wateja kununua maitaji ya mavazi ya watoto yakiwemo mabegi pia mambo mbali mbali kama pombe za kidunia katika duka lake jipya kufunguliwa mapema mwezi ujao la First Supper Market iliyopo mbezi mbeach kona ya Goba

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...