Wizara
ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imepokea nafasi za masomo ya
muda mrefu katika fani ya Sayansi kutoka Serikali ya Misri.
Masomo
hayo ambayo ni kwa ngazi ya Shahada ya
Uzamili na Uzamivu yatatolewa kwenye Chuo Kikuu cha Alexandria kilichopo nchini
Misri chini ya udhamini wa Mpango wa Bonde la Mto Nile (Nile Basin Initiative).
Mwisho
wa kuomba nafasi hizo ni tarehe 30 Mei 2019. Kwa maelezo zaidi kuhusu kozi hizo
na namna ya kuomba, tafadhali tembelea tovuti ifuatayo: www.nbs.alexu.edu.eg
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara
ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
10 Mei 2019
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...