Anaripoti Dixon Busagaga
MBUNGE wa Jimbo la Vunjo,  James Mbatia amesema anakusudia kupaza sauti juu ya kuanzishwa kwa somo linalohusu kujiandaa na Majanga “ Disaster Preparedness”  katika shule za msingi,sekondari na vyuo ili kuwaandaa wanafunzi kuweza kukabiliana na majanga pindi yanapotokea.

Kauli ya Mh Mbatia ambaye pia ni mtaalamu wa Majanga inakuja siku chache baada ya Mabweni mawili katika shule ya sekondari ya wasichana ya Ashira iliyopo Marangu mkoani Kilimanjaro kuungua moto na kuteketeza vitu mbalimbali yakiwemo magodoro,shuka na nguo za wanafunzi.

Tayari wadau mbalimbali wameendelea kujitokeza kutoa msaada wa kibinadamu kwa wanafunzi 73  ,waathirika wa ajali hiyo ya moto miongoni mwao ni Mbunge wa jimbo la Vunjo na Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi James Mbatia aliyekabidhi msaada wa mabegi 73 kwa ajili ya kuhifadhi nguo za wanafunzi hao.
 Mbunge wa Jimbo la Vunjo,James Mbatia akiwa ameongozana na Mkuu wa shule ya Sekondari ya Wasichana ya Ashira , Elizabeth Abdalah alipofika kutoa pole pamoja na msaada kwa wanafunzi waliathirika na ajali ya moto iliyoteketeza Sehemu ya Mabweni mawili katika shule katika shule ya sekondari ya wasichana ya Ashira iliyopo Marangu mkoani Kilimanjaro.



 Sehemu ya Mabweni ya Japan na Muungano yaliyoungua Moto hivi karibuni katika shule ya sekondari ya wasichana ya Ashira iliyopo Marangu mkoani Kilimanjaro.
 Mabaki ya nguo na vifaa mbalimbali vya wanafunzi baada ya moto kutekekeza sehemu ya Mabweni Katika shule ya Sekondari ya Wasichana ya Ashira iliyopo Marangu mkoani Kilimanjaro.
 Mbunge wa jimbo la Vunjo,James Mbatia akikabidhi msaada wa Mabegi kwa ajili ya kuhifadhi nguo kwa wanafunzi walioathirika na ajali ya moto katika shule ya sekondari ya wasichana ya Ashira iliyopo Marangu mkoani Kilimanjaro.

  Mbunge wa jimbo la Vunjo,James Mbatia akizungumza na wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Ashira wakati akitoa pole kwa wanafunzi hao


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...