VIONGOZI wa nchi za Kiarabu wameishutumu Iran na kuitaka kuacha kuingilia mahusiano ya nchi nyingine.

Kwa mujibu wa Mtandao wa DW umesema kuwa shutuma hizo nchi hizo wamezitoa wakati wakihitimisha mikutano miwili ya kilele ya dharura nchini Saudi Arabia baada ya mashambulizi kwenye ukanda wa Ghuba. Iran ililaumiwa kwa mashambulizi hayo.

Taarifa ya kuhitimisha mikutano hiyo imechapishwa mapema leo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya nchi za kiarabu, Arab League, Ahmed Aboul Gheit baada ya mkutano wa jumuia hiyo.

Mikutano ya jumuia hiyo pamoja na Baraza la ushirikiano wa mataifa ya Kiarabu, GCC katika Mji wa Mecca iliitishwa baada ya mashambulizi kwenye meli nne za mafuta katika Pwani ya Umoja wa Falme za Kiarabu, UAE na yale ya ndege zisizo na rubani kwenye mabomba ya mafuta nchini Saudi Arabia yaliyofanywa na waasi wa Houthi wa Yemen wanaoungwa mkono na Iran.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...