NA MWAMVUA MWINYI, KIBAHA

SHEIKH wa Mkoa wa Pwani,Khamis Mtupa ametoa rai kwa jamii inayojiweza kimapato,  kujitolea kuwasaidia watu wenye matatizo na wasiojiweza kwani ni njia mojawapo ya kujitengenezea na kujihifadhia twawabu ya kuingia peponi.

Aliyasema hayo wakati akifungua umoja wa Twariqa ,wilayani Kibaha ambazo ofisi yake ipo kata ya Kongowe Mtaa wa Mwambisi.

 Sheikh Mtupa aliwaeleza waumini wa dini ya kiislamu na wananchi kuwa mwanadamu akijihusisha na wenzake katika Twariqa ya kujitolea kusaidia wasiojiweza hujiandalia pepo. 

"Umoja huu wa twariqa ulioanzishwa mtaa wa Mwambisi kila anayeingia basi afahamu Twariqa inachukua dhamana ya yeye kufika peponi In jehanam firdaus Pepo ambayo kama tunazungumzia matokeo ya mtihani basi huyo mwanafunzi anakuwa amepata daraja la kwanza, 

"Hivyo ndugu zangu waislamu na wananchi kwa ujumla tujumuike na wenzetu katika umoja huu wa Twariqa ambao upo mahususi kwa ajili ya kusaidiana" alisema sheikh Mtupa.

Nae sheikh wa wilaya ya Kibaha,Said Mtonda alieleza, lengo la kuanzishwa kwa umoja huo wa Twariqa kwa wilaya ya Kibaha ni umoja wa kushirikiana kwa waumini wa dini ya kiislamu na wananchi katika kutoa msaada kwa waislamu wenzao na jamii pindi wanapopatwa na matatizo jambo la furaha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...