Na Derek Murusuri, Magomeni, Dar es Salaam
Sabato/Jumamosi 11 May 2019

#Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa: "Serikali ya awamu ya tano itaendelea kuheshimu uhuru wa kuabudu nchini."

#Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa: "Serikali yetu itaendelea kushirikiana na dini zote katika taifa letu ili kuleta utulivu, amani na umoja wa kitaifa. Kuja kwangu hapa katika Kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni kuabudu pamoja nanyi leo ni uthibitisho huo."

Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa: "Kitabu cha Ayubu 22:21 kinasema, "mjue sana Mungu ili uwe na amani; ndivyo mema yatakavyokujia."

#Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa: "Serikali yetu itaendelea kumtegemea Mungu katika kuwaletea watanzania maendeleo."

#Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa: "Nalipongeza kanisa la Waadventista wa Sabato katika kuandaa kitabu hiki cha Tumaini la Familia."

#Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa: "Kitabu hiki kitatusaidia kufundisha maadili bora."

#Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa: "Nawasihi, ili kujenga familia imara itakayosaidia kuwa na taifa imara, kitabu hiki kisomwe si na waadventista wasabato peke yenu, bali waislamu na wakristo wa madhehebu mengine pia." 

#Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa: "Taifa imara siku zote, msingi wake hutegemea familia imara"

#Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa: "Kitabu cha Ayubu 22:21 kinasema, mjue sana Mungu ili uwe na amani. Ndivyo mema yatakavyokujia. 

#Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa: Serikali inatambua mchango wenu muhimu katika kuhubiri neno la Mungu na kuwahudumia watanzania wote kwenye elimu, afya na maafa, bila ubaguzi.

#Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa: Nimetiwa moyo sana kuona mnajenga Kanisa kubwa na zuri sana. Watanzania tunaweza kufanya mambo makubwa pasipo kusubiri ufadhiri wa kutoka nje.

#Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa: Endeleeni kuwahimiza washiriki kutoa sadaka, zaka na kulipa kodi, ili kuendeleza kazi ya Mungu na vilevile kuchangia maendeleo ya taifa letu.*
Zawadi ya picha ya kuchorwa aliyozawadiwa Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kanisa la Waadventista Wasabato la Magomeni Mwembechai katika ibada ya kuadhimisha miaka 100 tangu Kanisa hilo lianzishe idara ya familia. Mchoraji ni Sethi Samuel KENGURU, mwenye makazi yake katika jiji la Arusha.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...