Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd. Shaaban Seif Mohamed Kulia na Mhadhiri Muandamizi wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar {SUZA} Dd. Zakia Mohamed Abubakar wakitia saini Mkataba wa kufanya Utafiti kugundua sababu zinazopelekea Zanzibar kuathiriwa na tatizo la mmongo’nyoko unaopelekea kudidimia kwa ardhi. Wa kwanza kulia aliyefika kushuhudia utiaji saini Mkataba huo ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Mohamed Aboud Mohamed.
Baadhi ya Wakurugenzi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nchi Ofisdi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Mohamed Aboud Mohamed akizungumza mara baada ya kumalizika kwa utiaji saini Mkataba huo.
Mhadhiri Muandamizi wa Chuo Kikuu cha Taifa
Zanzibar {SUZA} Dd. Zakia Mohamed Abubakar akielezea faraja yake
kutokana na Serikali Kuu kuwaamini kuwapa fursa ya kutumia ujuzi wao
katika masuala ya utafiti.
Picha na – OMPR – ZNZ.
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetiliana saini Mkataba na
Wataalamu wa chuo kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) ili kufanya tafiti
kugundua sababu zinazopelekea Zanzibar kuathiriwa na tatizo la
mmongo’nyoko unaopelekea kudidimia kwa ardhi katika baadhi ya maeneo
hasa wakati wa kipindi cha mvua kubwa zinaponyesha.
Utafifiti huo utakwenda sambamba na kuchunguza mbinu mbadala
zinazoweza kutumika katika kuondosha takataka zitokanazo na mali ghafi
za platiki ambazo zimekua chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira kwa
muda mrefu ndani ya Zanzibar hali inayosababisha athari juu ya mripuko
wa maradhi katika jamii.
Mkataba huo umetiwa Saini na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa
Rais wa Zanzibar Nd. Shaaban Seif Mohamed kwa upande wa Serikali na
Uongozi wa Chuo Kikuu ca Taifa Zanzibar ukatiwa na Mhadhiri Muandamizi
wake Dr. Zakia Mohamed Abubakar.
Akizungumza mara baada ya utiaji saini huo katika ukumbi wa Kamati ya
Sheria Baraza la wawakilishi Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa
Rais Mhe. Mohamed Aboud Mohamed alisema kitendo hicho kinachofanywa
na Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kitakuwa cha kihistoria ambacho
matokeo yake yatavinufaisha vizazi vya sasa na vile vijavyo.
Waziri Aboud alisema ni kipindi cha muda mrefu sasa Zanzibar imekuwa
ikikumbwa na tatizo la kudidimia kwa Aridhi katika maeneo mbali mbali
ya unguja hasa inapowadia kipindi cha mvua kubwa hali inayozusha hofu
kwa jamii na wakaazi wanaoishi katika maeneo yanayokubwa na kadhia
hiyo.
“Kumekuwepo na tatizo katika visiwa vyetu hivi kila mvua kubwa
zinaponyesha basi baadhi ya maeneo hudidimia na kutoa taharuki kwa
serikali pamoja na wakaazi wa maeneo hayo” Alisema Mhe. Aboud
Sambamba na hayo alisema kutiwa saini kwa mkataba wa kufanyika utafiti
kumempa imani na furaha kubwa kwani kitendo hicho kinaashiria
kulipatia ufumbuzi tatizo ambalo wananchi wamekua wakipatwa na wasi
wasi yanapotokea akitolea mfano kutokea kwa kudidimia kwa aridhi
katika eneo la Jango’ombe mshelishelini, Kwerekwe “C” Mombasa na Tukio
la juzi pembezoni mwa Madrasa Ismailia na Msikiti wa Mwanakwerekwe.
Akilitolea ufafanuzi tatizo la takataka pamoja na pemapasi Waziri
Aboud alisema watafiti hao wana kazi ya kulichunguza kwa kina jambo
ili kuja na suluhisho la kudumu juu ya mbinu mbadala zinazoweza
kutumika ili jamii iondokane na kadhia hiyo huku akiwa na imani kwamba
watafiti hao wataifanya kazi yao kwa ufasaha wa hali ya juu.
Nae Muhadhiri muandamizi kutoka chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar
{SUZA} Dk. Zakia Mohamed Abubakar alisema watafiti kutoka chuoni hapo
wanaishukuru serikali ya mapInduzi Zanzibar kwa kuwapa imani kubwa Ya
kuwapatia kazi ya kufanya tafiti mbili ile ya kudiDImia kwa ardhi na
tatizo la taka za plastiki na Pempasi na kuahidi kuwa wataifanya kazi
hiyo kwa uweledi mkubwa katika kutokomeza tatizo hilo.
Dk. Zakia alisema timu ya watalamu hao itafanya kazi kwa ustadi ili
kubaini kiini halisi cha tatizo hilo ili iwe rahisi kutoa maelekezo
kwa wananchi juu ya sababu zinazopelekea kutokea kwa matukio hayo.
Aidha alisema jamii inapaswa kuondosha hofu juu ya matukio hayo kwani
baadhi ya wakati hali hiyo inaweza kusababishwa na aina ya udogo au
kutembea kwa udongo chini ya ardhi.
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu kutoka Ofisi ya Makamu wa Pili wa
Rais Ndu. Abdalla Hassan Mitawi alisema serikali imeamua kufanya
tafiti hizo kusudi kubaini chanzo cha tatizo na alieleza kuwa matukio
ya utafiti huo yatakapowasilishwa itaisaidia serikali kufahamu hatua
za kuchukua kwa lengo la kupunguza athari hizo kwa wananchi wake.
Naibu katibu Mitawi Alisema matukio ya tafiti kwa upande wa matumizi
ya plastiki na pempasi yataiwezesha serikali kubuni njia mbadala za
kutumia ili kuviepushia visiwa vya Zanzibar kukumbwa na athari
zinazoweza kuepukika.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa utafifiti na shahada za juu Dk.
Makame Omar Makame alifafanua kuwa timu ya watalamu hao itajitahidi
kuzifanya tafiti hizo kwa umahiri ili ije maelezo sahihi ndani ya
kipindi cha muda mfupi kutokana na tatizo la taka za plastiki na
pempasi kuzagaa kwa wingi mitaani hali inayosababisha kipindi cha mvua
kubwa maji kutuwana na kuleta athari katika sehemu za makaazi ya
wananchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...