NA MWAMVUA MWINYI,KIBAHA

RASHID Said ( 17 )amefariki dunia baada ya kudaiwa kupigwa jiwe lililompata kichwani eneo la kisogoni na mwenzake ambae ni mwanafunzi wa shule ya sekondari Nyumbu huko Kibaha mkoani Pwani.

Kufuatia kutokea kwa tukio hilo, jeshi la polisi mkoani Pwani,linamshikilia mwanafunzi huyo ili kuendelea na taratibu za kisheria.

Kamanda wa polisi mkoani humo ,Wankyo Nyigesa aliwaambia waandishi wa habari kwamba,chanzo ni ugomvi uliotokea baina ya vijana hao.

Alieleza,,juni 7 mwaka huu maeneo ya Pichandege marehemu alijeruhiwa kwa kupigwa jiwe baada ya tukio hilo alipelekwa katika hospital ya rufaa ya Tumbi kwa matibabu ambapo juni 8 alifariki dunia.

"Mtuhumiwa siku ya tukio alikuwa akirudi nyumbani na alikutana na vijana wenzake akiwemo marehemu wakimzuia asipite na ndipo marehemu alianza kumtukana mtuhumiwa "

Wankyo alieleza,mtuhumiwa alifanya jitihada za kukimbia lakini kabla hajafika mbali marehemu alimrushia jiwe lililompiga ubavuni hivyo mtuhumiwa kuamua kumrushia jiwe marehemu lililompata kichwani kisogoni.

Mwili wa marehemu umepelekwa hospital ya taifa ya Muhimbili kwa uchunguzi zaidi .

Jeshi la polisi Pwani linatoa wito kwa jamii kuacha kujichukulia sheria mkononi ili kujiepusha na matatizo ama kujikuta wakichukuliwa hatua za kisheria.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...