Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Injinia Stella Manyanya akitoa hotuba yake wakati wa Mahafali ya chama cha wanafunzi wa Kiswahili Afrika mashariki tawi la Makumira
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Injinia Stella Manyanya akisaini kitabu cha wageni walipowasili kwenye Mahafali ya chama cha wanafunzi wa Kiswahili Afrika mashariki tawi la Makumira wilaya Arumeru picha zote na Ahmed Mahmoud Arumeru.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Jerry Muro akitoa nasaha zake kwenye Mahafali ya chama cha wanafunzi wa Kiswahili Afrika mashariki tawi la Makumira picha na Ahmed Mahmoud Arumeru


Na Ahmed Mahmoud Arumeru

Mahakama zimetakiwa kuangalia namna ya kukitumia Kiswahili wakati mwananchi anapokata rufaa kwenye mahakama za rufaa badala ya utaratibu unaotumika sasa.

Ambapo pia Watanzania wametakiwa kutumia fursa ya kukitangaza na kueneza Lugha adhimu kwa kukienzi Kiswahili ili kitupatie maarifa zaidi na kuzitumia lugha nyingine kukuza mawasiliano kote ulimwenguni.

Akiongea kwenye Mahafali ya 12 ya CHAWAKITUMA na Kongamano la Kiswahili kwenye Chuo cha Makumira Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Injinia Stella Manyanya alisema kuwa Kiswahili ni kidhibiti kasi katika Biashara kwani Biashara inatija na faida hivyo kujiamini ni sehemu ya Biashara kwa kuwa mawasiliano yapo kati yenu.

Amesema kuwa anahidi serikali ya awamu ya tano ni sikivu na itasikiliza kwa kushika lugha yetu kwani lugha hiyo ni bidhaa na fursa ya kiuchumi kwa kuinua mkono kukinadi Kiswahili.

Kuna changamoto kutokana na kutotumika kwa lugha ya Kiswahili kwenye Rufaa kwani eneo hilo zinaonyesha litawanyima wadawaa haki kwa kutumika lugha ya kuongeza “Lugha ya Kiswahili ni bidhaa Bora ndio maana Mh.rais kila mahali amekuwa akikinadi kwenye mataifa mbali mbali ili kuweza kutoa walimu na hivyo fursa ya Kiswahili kukua kwa kukitangaza hata kwenye bidhaa zetu”
 
Amewataka kuwa wahitimu hao kuchangamkia fursa za kufundisha Kiswahili kwani wanaweza kuitumia nafasi hiyo kueneza upendo kwenye maeneo yenye vurugu kwani lugha hiyo inamchango wa kuweza kupatanisha.
Amesema kuwa mabango ya usalama Barabarani yameboreshwa kwa kutumia lugha ya Kiswahili namshukuru sana na kongole wadau wa Kiswahili kwani lugha hiyo hapa nchini ni lugha rasmi.

Kupitia viwanda tunaweza bidhaa zetu watu kununua kwa haki sehemu hii ni nafasi ya sehemu ya viwanda katika mchango wake katika kukiuza .
Akiongea kwenye Mahafali hayo yalioenda sambamba na Kongamano la Kiswahili kwenye chuo cha Makumira Makamu Mkuu wa Chuo cha Makumira Utawala Prof. Joseph Parsalaw Alisema kuwa Kiswahili ni tunu na fursa ya kuongeza mawasiliano na kuwataka watanzania kukienzi.

Naye Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro alisema kuwa aliwataka wahitimu kuangalia namna nzuri ya kukilea na kujifunza Kiswahili tujipange kwani wenzetu wanatumia nafasi na kujitangaza kiswahili kipo nchini mwao nanyi wanazuoni ndio wakuondoa ombwe hilo kwa dunia kujua asili ya Kiswahili.

“Haya yote vijana tusimame tuinuke kwani hatma ya taifa hili ipo mikononi mwetu kwa kuenda kufundisha kukitangaza na kuwa mabalozi wazuri wa kukitangaza Kiswahili chetu”


Alisema Tunamshukuru mh.rais ameendelea kujipambanua na kukitangaza Kiswahili fikra sahihi huja wakati sahihi na mkumbuke lugha hii ni ya tatu inayopendwa na kutamalaki barani Afrika kwa kufanya shughuli za mawasiliano.
Alisema kuwa Wakongo wanapoingia nchi za jumuiya ya Afrika mashariki ni fursa nzuri kuitumia kwa kutoka na kwenda kujionea fursa na kuacha kusikiliza ambayo hawajajionea kabla hawajafik

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...