Halmashauri ya Jiji la Mwanza inatarajia kuanza utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ambayo ni pamoja na ujenzi wa soko kuu, stendi ya mabasi Nyegesi pamoja na kituo cha maegesho ya magari makubwa Buhongwa ambapo miradi hiyo itaongeza ukusanyaji wa mapato ya halmashauri hiyo.
Hayo yalisemwa jana Juni 05, 2019 na Mkurugenzi wa Jiji hilo, Kiomoni Kibamba wakati akizungumza kwenye kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika eneo la Soko Kuu.
"Kutakuwa na "parking" ya magari zaidi ya 500 kwa wakati mmoja chini ya ardhi...ukiingia na hela unatumbukiza kwenye mashine, inakupa chenchi..." alisema Kibamba.
Tazama video hapa chini
PIA SOMA>>> Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani 2019


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...