Meya Mwenda ametoa ahadi hiyo wakati wa futari aliyoiandaa maalumu kwa ajili ya walimu hao, wakiwemo maustadhi na Masheikh wa Misikiti iliyopo katika wilayani Kinondoni , akiitikia ombi la Sheikh wa Wilaya ya Kinondoni Mohammed Mhenga aliyemuomba kufadhili mafunzo hayo.
Katika futari hiyo aliyokuwa ameiandaa katika makazi yake Mikocheni Dar es Salaam, Mwenda amesema mafunzo kwa walimu hao ni jambo asiloweza kulipa ugumu kwa kuwa anatambua thamani yao na hasa katika uenezaji na uendelezaji wa dini hiyo.
“ Natambua kazi nzuri mnayoifanya katika kufundisha dini ya Uislam hasa kwa watoto wetu na jamii ya watu wengine, nimelipokea suala hili na nipo tayari kushirikiana nanyi wakati wowote mtakaponiambia kuwa mpo tayari” amesema Mwenda.
Aidha ameongeza kitendo chake na kuwaalika walimu hao na kufuturu nao pamoja, kimelenga kuwatambua na kuthamini mchango wao mkubwa wanaoutoa kuiendeleza Quran ambayo ilishushwa ndani ya mwezi wa Ramadhan maalumu kwa ajili ya waumini wa dini ya kiislam pamoja na waamini wengine.
“Niwapongeze kwa kazi nzuri mnayoifanya kuindeleza dini hii, kwa hakika mnabeba thawabu kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu, naamini siku moja atawalipa kama siyo hapa duniani basi akhera” ameeleza Meya huyo Mstaafu.
Awali Sheikh Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mohammed Mhenga mbali na kumpongeza Mwenda kwa hatua yake ya kufuturu na walimu hao, amewataka walimu hao kuzidisha elimu wanayoitoa kwa vijana kwa lengo la kuzidi kuieneza dini hiyo.
Pia amesema kumalizika kwa mwezi mtukufu kusiwafanya waislam kubadirika na kugeuka kutenda matendo yenye kumchukiza Mungu na badala yake waendelee kusimama kikamilifu na kumuabudu mwakati wote


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...