Kampuni ya simu ya TECNO mobile inawakaribisha wateja wake kununua simu mpya iliyozinduliwa hivi karibuni aina ya TECNO SPARK 3 na kujishindia zawadi kemkem ikiwemo pikipiki mpya.
Promotion hiyo iliyopewa jina la boda la spark 3 inaanza kwa mkoa wa dar es salaam kisha kuenea mikoa mingine hapo baadae, mteja atakaenunua TECNO spark 3 kwenye maduka maalumu ya TECNO yenye promotion hiyo atapewa nafasi ya kuondoka na zawadi za papo kwa papo kama power bank yenye mAh 5000 na pamoja data cable,
TECNO Spark 3 ni simu ya kijanja yenye uwezo mkubwa wa kupiga picha pamoja na kufanya vitu mbali mbali mitandaoni imezinduliwa takribani mwezi mmoja ikiwa ndio simu inayofanya vizuri zaidi kwa upande wa simu janja za kipato cha kati.
TECNO SPARK 3 ina ubora wa kamera yenye megapixel 13, huku mtumiaji anapata nafasi ya kuifadhi vitu vyake kwenye GB 16 za memory ya ndani na muonekano wake ni wakijanja na ndio maana inafanya vizuri sokoni,
Mshindi wa pikipiki atapatikana mwisho wa mwezi wa sita kwa njia ya bahati nasibu itakayo chezeshwa live kupitia mitandao ya kijamii ya TECNO mobile hasa Instagram
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...