Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
Mamlaka ya Bandari Tanzania(TPA) Kwa upande wa Maziwa makuu katika eneo la Ziwa Victoria imewakaribisha wadau na wafanyabishara wa majini katika ziwa hilo kutumia Cherezo ya ndani ya maji iliyopo katika bandari ya Mwanza hili kuweza kukarabati meliz zao kwa ufanisi.
Hayo yamesemwa na Kaimu Meneja wa Bandari ya Mwanza Bw. Geoffrey Lwesya wakati akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Mwanza ambao wapo katika ziara ya kutembelea na kutangaza miradi ya maendeleo ya bandari zilizo katika Ziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa
" Nawaomba wafanyabiashara wenye meli zao katika ziwa Victoria waje wafanye matengenezo kwa kutumia hii cherezo kwa ajili ya usalama wa vyombo vyao ,kumekuwa na maneno maneno juu ya gharama za kutumia hii cherezo ni kubwa lakini ukweli ninao waambia kuwa gharama zetu ni nafuu sana ambazo kila mtu anayemiliki meli katika ziwa hili anaweza kuzimudu"
Kaimu Meneja wa Bandari ya Mwanza,Geoffrey Lwesya akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Mwanza ambao wapo katika ziara ya kutembelea na kutangaza miradi ya maendeleo ya bandari zilizo katika Ziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa
Kaimu Meneja wa Bandari ya Mwanza,Geoffrey Lwesya akiwaonyesha sehemu ya Cherezo mpya inayojengwa na Serikali ya awamu ya tano ambayo ipo katika Bandari ya Mwanza
Sehemu ya Cherezo Mpya inayojengwa katika Bandari ya Mwanza ambapo ni moja ya maboresho ya bandari hiyo yanayofanywa na Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dr. John Pombe Magufuli
Kaimu Meneja wa Bandari ya Mwanza, Geoffrey Lwesya akiongozana na waandishi wa habari leo jijini Mwanza ambao wapo katik ziara ya kutembelea na kutangaza miradi ya maendeleo ya bandari zilizo katika Ziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa
Sehemu ya Makuli wanaopakua Mizigo katika Bandari ya Mwanza wakipakua mzigo wa Mbao unaoshushwa kwenye meli tayari kwa ajili ya kusafirishwa.
Cherezo ya Ndani ya Maji iliyopo katika Ziwa Victoria inayomilikiwa na Mamlaka ya Bnadari Tanzania yenye urefu wa Km 110 kama inayoonekana kwa juu ikiwa aijazama kwenye maji.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...