Editha Edward-Tabora
Wafanya biashara wilayani Nzega mjini Mkoani Tabora wamelalamikia mwingiliano wa kimamlaka wa ukusanyajj wa ushuru wa huduma kati ya Halmashauri ya wilaya ya Nzega na mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) ambayo yamekuwa yakiwaathiri kibiashara wilayani humo
Yamesemwa hayo katika kikao kilichoitishwa na meneja wa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Tabora Thomas Masese ambacho alikiitisha kwa ajili ya kupokea ushauri na kero kutoka kwa Wafanyabiashara wa wilayani humo wakaitumia fursa hiyo kulalamikia mwingiliano wa ukusanyaji wa ushuru baina ya Halmashauri ya mji na TRA
Baadhi ya Wafanyabiashara hao akiwemo self Haruna wametaka kujua ni nani mwenye dhamana ya kukusanya ushuru kati ya TRA na Halmashauri ya mji na kwa viwango gani vya malipo na kwa biashara zipi ambazo wanapaswa kulipia ili kuondoa mkanganyiko huo
Katika kikao hicho Wafanyabiashara hao wameiomba TRA kuongeza timu ya Maafisa ili kuharakisha kutembelea biashara na kutoa ukadiliaji wa ulipaji wa kodi pamoja na kuhimiza kampuni iliyopewa jukumu la kusambaza Mashine za EFD toka mwaka juzi kupeleka Mashine hizo
Akijibu malalamiko hayo meneja wa mamlaka ya Mapato TRA mkoa wa Tabora Thomas Masese amebainisha utofauti wa ukusanyaji wa ushuru kati ya taasisi yake na Halmashauri kwa kuchukua asilimia kutoka kwa Wafanyabiashara na kuwa ahidi Wafanyabiashara hao kukutana na Mkurugenzi ili kuweza kuondoa usumbufu huo.
Pichani ni Meneja wa TRA Tabora Thomas Masese akizungumza na Wafanyabiashara katika kikao kilichofanyika mjini Nzega.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...