Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Balozi Joseph Sokoine leo amefungua Mafunzo ya Msasa ya Uwezeshaji kuhusu Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame ya nch (LDFS), yanayofanyika katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Morogoro
Sehemu ya Washiriki wa Mafunzo ya Msasa ya kuhusu Uwezeshaji Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame ya nchi (ldfs),wakiwa kwenye makundi kufanya uchambuzi yakinifu wa mimea na ikolojia shambani katika Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) mkoani Morogoro. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Balozi Joseph Sokoine akizungumza na Profesa Henry Mahoo wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (katikati) na Dkt. Moses Temi Mkufunzi Mkuu wa Shamba Darasa katika kituo cha Mafunzo ya Kilimo Nkindo wilaya ya Mvomero mara baada ya kufunguaMafunzo ya Msasa ya Uwezeshaji kuhusu Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame ya nchi (LDFS), yanayofanyika katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Morogoro 

……………………………………………. 

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Balozi Joseph Sokoine leo amefungua Mafunzo ya Msasa ya Uwezeshaji kuhusu Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame nchini (ldfs), katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Morogoro.

“Ni matumaini yangu kuwa elimu na ufahamu mtakauopata kupitia mafunzo haya, mtaitumia katika kufanikisha uanzishaji wa mashamba darasa katika maeneo ya mradi” alisema Balozi Sokoine.Mafunzo hayo ya siku 5 yanalenga kujenga uwezo kwa washiriki katika uanzishaji wa mashamba darasa katika vijiji na shehia ambako mradi wa LDFS unatekelezwa.

Tanzania kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wamekuwa wakitekeleza miradi inayolenga kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo na mifugo kwa kusogeza karibu teknolojia kwa wakulima. Lengo likiwa ni kuongeza usalama wa chakula na kuongeza kipato cha jamii. Mradi wa LDFS ambao umeandaa mafunzo haya ni mfano wa juhudi hizo za Serikali. Juhudi hizi zinahusisha uingizaji na matumizi ya teknolojia mpya ikiwemo matumizi sahihi ya mbolea, mbegu zenye ubora; uboreshaji wa nyanda za malisho; utoaji wa huduma za ugani na mafunzo kupitia shamba darasa. Juhudi hizi zote zina lengo la urejesha ardhi iliyoharibika ili iweze kuendelea kuzalisha mazao ya kilimo, mifugo na misitu.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi huo wa LDFS Bw. Joseph Kihaule amesema mradi huo utajumuisha na uanzishwaji wa mashamba darasa 100.
Wawezeshaji wa mradi huo ni Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO), Chuo cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na Wakala wa Taifa wa Mbegu za Miti Tanzania (TTSA) ambapo washiriki wa mafunzo hayo wametoka Wizara za Kilimo, Maliasili na Utalii, Maji, Mifugo na Uvuvi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Idara ya Mazingira, Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar. Aidha, washiriki wengine ni kutoka katika Halmashauri zinazotekeleza Mradi za Mkalama, Micheweni, Magu, Nzega na Kondoa, pamoja waalikwa rasmi Daktari Moses Temi na Bwana Charles Mjema. 
Sehemu ya Wajumbe walioshiriki Mafunzo ya Msasa ya Uwezeshaji kuhusu Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame ya nchi (LDFS), yanayofanyika katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Morogoro . (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Balozi Joseph Sokoine (katikati)akihutubia wakati wa ufunguzi Mafunzo ya Msasa ya Uwezeshaji kuhusu Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame ya nchini (LDFS), yanayofanyika katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Morogoro, wengine pichani ni Mratibu wa Mradi huo Bw. Joseph Kihaule (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Mazingira Bw. Faraja Ngerageza. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Sehemu ya Wajumbe walioshiriki Mafunzo ya Msasa ya Uwezeshaji kuhusu Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame ya nchi (LDFS), yanayofanyika katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Morogoro . (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Sehemu ya Washiriki wa Mafunzo ya Msasa ya kuhusu Uwezeshaji Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame ya nchi (ldfs),wakiwa kwenye uchambuzi yakinifu wa mimea na ikolojia shambani katika Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) mkoani Morogoro (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Sehemu ya Washiriki wa Mafunzo ya Msasa ya kuhusu Uwezeshaji Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame ya nchi (ldfs),wakiwa kwenye makundi kufanya uchambuzi yakinifu wa mimea na ikolojia shambani katika Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) mkoani Morogoro. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...