Sehemu ya Ziwa Tanganyika likionekana likiwa limetulia 
Sehemu ya eneo itakapojengwa Bandari ya Kisasa ya Karema wilayani Tanganyika
Baadhi ya viongozi wa CCM mkoa wa Katavi na watumishi wa serikali wakiwa na Balozi Silima katika ufukwe wa Ziwa Tanganyika

************* 

Na Mwandishi wetu, Katavi 

Mradi wa ujenzi wa bandari ya kisasa utakaogharimu kiasi cha shilingi bilioni 65 katika kata ya Karema wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi utawezesha kufungua lango kuu la biashara kati ya mkoa huo na nchi jirani ya Kongo DRC kutokana na nchi hiyo kutegemea chakula kutoka mkoani katavi ambapo kwa sasa kinasafirishwa kwa kutumia majahazi 

Akizungumza na Wanahabari Katibu tarafa wa tarafa ya Karema Bi. Zawadi Mirambo,amesema kuwa tayari wametenga eneo la ukubwa wa mita 1000 kwa ajili ya ujenzi wa bandari hiyo hivyo mita 500 ni kwa ajili ya ujenzi wa bandari hiyo na mita nyingine 500 ni ziada itakayoendelezwa baadae ambapo wananchi waliopo katika eneo hilo wapo tayari kupisha mradi mara watakapolipwa fidia. 

Naye Afisa Tawala wa wilaya ya Tanganyika Bwana Reginald Mhango amesema tayari serikali imekwisha idhinisha kiasi cha shilingi bilioni 25 kwa ajili ya kuanza kwa ujenzi huo. 

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Mpanda Vijijini Bw. Selemani Kakoso amesema bandari hiyo ya kisasa itaboresha uchumi wa watu wa Katavi na nchi kwa ujumla kutokana na upande wa Kongo Kusini kupokea kiasi kikubwa cha chakula kutoka mkoani Katavi. 

“Si Mahindi na Mchele tu hata Kitunguu wanachopikia Kongo kinatoka Katavi”. Amesema mbunge huyo. 

Katibu wa Halmashauri kuu ya Taifa Bw. Pereira Silima ambaye pia ni mlezi wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Katavi amefika kukagua eneo itakapojengwa bandari hiyo ambapo amewataka viongozi kuwa makini katika usimamizi wa utoaji wa fidia kwa wananchi na usimamizi wa mradi wenyewe.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...