Kipekee naomba nimshukuru Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) Robert Boaz kupitia Kitengo cha CYBER CRIME kwa kufanikisha kumnasa mtuhumiwa wa utapeli ambae amekua akijipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Amefungua ukurasa Facebook kwa jina langu na kudanganya watu kuwa ninatoa mikopo Kwa njia ya Saccos / Viccoba na hivyo wamtumie fedha Huyu Mtuhumiwa kwenye picha kupitia namba 0713924045 jina lake ni Abdalah Mbanjo ya kuomba mikopo na akiba ya asilimia kumi ya mikopo wanayoomba.

Kwa mara nyingine napenda kuijulisha jamii kwamba sina taasisi yoyote ile inayotoa mikopo na watoe taarifa kituo chochote cha polisi iwapo mtu yoyote au taasisi yoyote itatumia jina langu au ofisi ya DC wa Kisarawe kujipatia fedha Kwa njia ya udanganyifu.

Baada ya mtuhumiwa huyu kutiwa nguvuni ilibainika kuwa yapo makundi mengine mengi ambayo yanatumia jina langu kujipatia fedha Kwa njia ya udanganyifu.

Na yote tumeshafahamu yalipo. Nalishukuru Jeshi la Polisi Kwa kuwa wamejipanga kuwasaka popote walipo nchini na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria na wote wanaotumia jina langu vibaya kwenye mitandao tutawachukulia hatua kali.

Mwisho ila sio kwa umuhimu Namshukuru na Kumpongeza IGP Sirro kwa kuwa na jeshi la polisi makini lenye kufanya kazi kwa weledi.- Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo.
Mtuhumiwa  Abdalah Mbanjo 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...