WAZIRI wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola, akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Msingi Karukekere, Jimboni kwake Mwibara, Wilayani Bunda, leo. Lugola aliwataka wanafunzi hao kupenda masomo na kuacha utoro, na pia aliliagiza Jeshi la Polisi wilayani huko, kuwakamata wazazi wanaowatumia wanafunzi katika shughuli za kilimo na mifugo na kuwasababishia kukatisha masomo yao. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola, akimuhoji Mratibu Elimu Kata ya Namuhura, Jimbo la Mwibara, Wilaya ya Bunda (wapili kushoto), Ibrahimu Kadashali, kuhusu uwepo wa taarifa za wanafunzi watoro, pamoja na wazazi kuwatumia wanafunzi katika shughuli za kilimo na mifugo na kuwasababishia kukatisha masomo yao. Kushoto ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Karukekere, Charles Manyama. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola, akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Karukekere, Jimboni kwake Mwibara, Wilayani Bunda, leo. Lugola aliliagiza Jeshi la Polisi wilayani humo, kuwakamata wazazi wanaowatumia wanafunzi katika shughuli za kilimo na mifugo na kuwasababishia kukatisha masomo yao. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...