Tanzania inatarajia kuwa mwenyeji na mwenyekiti wa mkutano wa 39 wa jumuiya ya maendeleo ya Kusini mwa Afrika SADC utakaofanyika mwezi Agosti mwaka 2019 jijini Dar es salaam. Mkutano huo utatanguliwa na vikao vya awali kwaajili ya maandalizi na kutangulia kwa wiki ya maonyesho ya bidhaa za ndani ujulikanao kama wiki ya viwanda ya SADC 22-26 Julai. Mkutano huo utahudhuriwa na viongozi wa nchi 16 zinazounda jumuiya ya SADC. Mara ya mwisho nchi ya Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano huo ilikuwa mwaka 2003 ambapo Rais Benjamini Mkapa alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa jumuiya hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...