Na Charles James, Michuzi TV
Naibu
Waziri wa Maji, Mhe Jumaa Aweso amewataka Mameneja wa Mikoa na Wilaya
wa Wakala wa Majisafi, Usafi na Mazingira Vijijini kufanya kazi kwa
weledi na kuhakikisha wanaondoa changamoto za Maji katika maeneo yao.
Mhe
Aweso ameyasema hayo wakati alipokutana na Mameneja hao jijini Dodoma
ambapo amesema kwa sasa Wizara hiyo imeunda kitengo cha usanifu ambacho
kitasaidia katika kuangalia upya usanifu, mikataba na gharama
zinazowekwa na wakandarasi kabla ya ujenzi wa miradi.
Amewataka
Mameneja hao kutumia weledi na taaluma zao kuhakikisha wanamtua mama
ndoo kichwani na kuwataka kuacha mambo ya hovyo yaliyokuepo awali.
"
Katika ziara zangu zote katika maeneo mbalimbali nimekua mkali sana kwa
wahandisi na wakandarasi, baadhi ya wataalamu wametuangusha kwa kutumia
miradi kujipatia fedha, nimejionea mwenyewe miradi mingi wakishindwa
kuimaliza kwa wakati. Wakandarasi hawa hatuwezi kuwavumilia hata kidogo.
"
Mhe Rais ametuamini sana katika nafasi hizi tulizoteuliwa, ni jukumu
letu kumsaidia kazi na kutumia taaluma zetu kuhakikisha upatikanaji wa
maji kwa wananchi waliopo vijijini inafikiwa kwa asilimia 85 au zaidi
ifikapo mwaka 2020," amesema Mhe Aweso.
Amewataka
Mameneja hao kutosubiri Waziri au Katibu Mkuu kufika katika maeneo yao
ya kazi na kuwaonesha changamoto badala yake waunde mikakati ya
kuwawezesha kufikia maeneo yenye changamoto ya Maji ili waweze kuitatua.
Awali
akimkaribisha Naibu Waziri, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Prof Kitila
Mkumbo amesema malengo ya Wizara hiyo ni kuongeza upatikanaji wa Maji
kufikia asilimia 84 kutoka asilimia 64 kwa maeneo ya Vijijini, lakini
pia wakifikia asilimia 95 kutoka asilimia 84 kwa maeneo ya Mjini.
"
Tumekua tukiwekeza sana kwenye miradi mipya lakini kama tukiongeza
nguvu na kumaliza miradi ambayo imekwishaanza na kuanza kufanya basi
tungekua mbali sana hivyo katika bajeti zetu lazima tupange bajeti zetu
Katika kukarabati miradi ya zamani.
"
Mhe Naibu Waziri kazi kubwa na ya haraka kufanywa na RUWASA ni kujenga
imani kubwa kwa Mhe Rais na Wananchi, na imani hiyo itajengwa na
wahandisi hawa kwa kuhakikisha miradi ya wananchi inafanya kazi lakini
kubwa zaidi ni kumaliza tatizo la Maji," amesema Prof Mkumbo.
Naibu
Waziri wa Maji, Mhe Jumaa Aweso akizungumza na Mameneja wa RUWASA kwa
ngazi ya Mikoa na Wilaya (hawapo pichani) katika mkutano uliofanyika
jijini Dodoma.
Katibu
Mkuu Wizara ya Maji, Prof Kitila Mkumbo akitoa neno katika kikao cha
Mameneja wa RUWASA kwa ngazi ya Mikoa na Wilaya jijini Dodoma.
Mameneja
wa RUWASA kwa ngazi za Mikoa na Wilaya wakiwa katika ukumbi wa Chuo cha
Mipango Jijini Dodoma walipokutana na Naibu Waziri wa Maji, Mhe Jumaa
Aweso.
Naibu
Waziri wa Maji, Mhe Jumaa Aweso (katikati) akiwa Katika picha ya Pamoja
na watendaji wa Wizara hiyo na Mameneja wa RUWASA kwa ngazi za Mikoa na
Wilaya jijini Dodoma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...