Mshindi wa kwanza katika mashindano hayo Fred Chacha kutoka Geita(katikati) akivaa kofia ngumu ya pikipiki wakati wa kukabidhiwa pikipiki yake aliyoshinda kupitia michezo ya bahati nasibu kwa njia ya tovuti na maduka ya kampuni hiyo yaliyofanyika katika ofisi zao leo jijini Dar es Salaam.
Mshindi wa kwanza katika mashindano hayo Fred Chacha kutoka Geita akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhiwa pikipiki mpya aliyoshinda kwenye mchezo ya bahati nasibu kwa njia ya tovuti na maduka ya kampuni ya Parimatch leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi muendeshaji wa Paramatch Tumaini Maligana.
Wafanyakazi wa Paramatch wakiwa kwenye picha ya pamoja na washindi 10 kutoka Mikoa mbalimbali nchini walokabidhiwa zawadi zao leo katika ofisi ya Mpuni hiyo leo jijini Dar es Salaam.
KAMPUNI ya Parimatch ambayo inajihusisha na michezo ya bahati nasibu kwa njia ya tovuti na maduka imepata washindi 10 kutoka Mikoa mbalimbali nchini na kukabidhi zawadi hizo kwa washindi hao.
Akizungumza katika hafla hiyo Mkurugenzi muendeshaji wa Paramatch Tumaini Maligana kampuni hiyo ambayo ni mpya na ya kisasa zaidi inaendesha michezo hiyo ya bahati nasibu kwa gharama ndogo zaidi ya shilingi 300 pekee.
Amesema kuwa wana maduka 12 ambayo yanatumia mbinu za kisasa katika uendeshaji wa michezo hiyo na wateja wanaweza kubeti hata mechi moja kwa gharama nafuu.
"Kampuni yetu tunaiendesha kisasa zaidi na hiyo ni kutokana na ukuaji wa teknolojia, tunapatikana kwa njia ya mtandao ya www.parimatch.co.tz na tunatumia kompyuta katika kuendesha michezo hiyo ya bahati nasibu na sio karatasi kama ilivyozoeleka" ameeleza Maligana.
Aidha amesema kuwa michezo ya kubahatisha kwao ni burudani na sio ajira kama inavyotafsiriwa na baadhi ya watu na wanaendesha michezo hiyo kwa ustaarabu wa hali ya juu.
Washindi hao waliopatikana kupitia mbio za Afcon wamejishindia zawadi mbalimbali ambapo mshindi wa kwanza amejishindia pikipiki, mshindi wa pili na watatu wamejishindia Smart TV na mshindi wa nne hadi kumi wamejishindia simu za kisasa za mkononi (smart phone.)
Mshindi wa kwanza katika mashindano hayo Fred Chacha kutoka Geita ambaye amejishindia pikipiki ameeleza kufurahishwa na namna mchezo huo ulivyoendeshwa hadi akaibuka mshindi na kujishindia pikipiki ambayo itampa ajira na amewashauri vijana wengine kutumia michezo hiyo kama burudani na sio ajira kama ilivyozoeleka.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...