RC Katavi , Mhe. Homera ameipongeza Halmashauri ya Mpimbwe kwa mwenenendo mzuri wa Ujenzi wa Hospitali ya wilaya kwa kufikia 87%.

Aidha, RC Homera amewapongeza kutokana na kasi kubwa ya ujenzi wakiongozwa na mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo ndugu Erasto Siwale ,aidha RC Homera amempongeza DED Erasto kwa kuwa msimamizi mahiri wa miradi na kuwaunganisha watumishi kuwa kitu kimoja katika halmashauri hiyo.

Hospitali hii inajengwa kwa Tsh Bilion 1.5. Mhe. Homera amewapongeza pia wafanyakazi na mafundi wanaoijenga hospitali hiyo na kuwataka waendelee kuwa wazalendo na kutotumia saruji na vifaa vingine kinyume na matakwa ya serikali.

Hata hivyo, RC Homera aliwaeleza wananchi waliokuwa hospitalini hapo kuwa ujenzi wa Hospitali hizo za mkoa mzima wa Katavi ni Jitihada za serikali ya CCM ya awamu ya Tano katika kutekeleza ilani yake ya mwaka 2015-2020  ibara ya 49,50 inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli ikisimamiwa vyema na waziri wa Nchi Ofisi Ya Rais Tamisemi Mhe Suleiman Jafo.

RC Homera amewataka wananchi na mafundi kuhakikisha Hospitali inakamilika kwa wakati ili waendelelee kufurahia matunda yanayotokana na serikali ya awamu ya tano.

 Lakini pia RC Homera amewahakikishia wananchi wa Halmashauri ya Mpimbwe wilayani Mlele mkoani Katavi ujenzi wa barabara kiwango cha lami KM 1.7-Mpaka 2 kwa Bajeti ya  mwaka 2019/2020 Katika Mji wa Uservya chini ya wakala wa Barabara Tanzania ,Tanroad. 

pia hayo yatafanyika sambamba na uanzishwaji wa Benki mojawapo katika mji huo ambao una uzalishaji mkubwa wa mazao ya biashara na chakula pamoja na Kata ya majimoto mkoani Katavi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...