Na Mwandishi wetu Mihambwe

Afisa Tarafa Mihambwe *Ndugu Emmanuel Shilatu* hajaridhishwa na ujenzi mradi wa ghala uliotumia Tsh. Milioni 40 lakini umeshindwa kukamilika na kuiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kufanya uchunguzi mara moja juu ya ujenzi huo na namna fedha hizo zilivyotumika.

Gavana Shilatu aliyasema hayo alipotembelea ghala hilo lililopo Kijiji cha Kitama Shuleni kata ya Kitama na kusikitishwa namna ambavyo fedha nyingi zikitajwa kutumika huku mradi ukiwa haujafika ukamilifu tarajiwa kiasi kinachopelekea kijiji kukosa mapato jambo ambalo ni kero kwa Wanakijiji waliokuja kulalamika kwa Afisa Tarafa huyo.

*”Serikali imetoa fedha tangu 2012 lakini mpaka sasa mradi haujakamilika na hivyo kunapelekea mapato yanakosekana ambayo yangesaidia kuleta maendeleo kijijini na maeneo mengineyo pia. Hili halikubaliki hata kidogo, naiagiza TAKUKURU kuanza uchunguzi mara moja juu ya ujenzi huu wa ghala.”* Alisisitiza Gavana Shilatu.

Mradi huo wa ujenzi wa ghala lililopo eneo la Kitama Farmers Group kwenye kijiji cha Kitama Shuleni ulianza tangu mwaka 2012 lakini hadi Leo hii haujakamilika na hivyo kukosesha Serikali mapato.

Katika ziara hiyo Gavana Shilatu aliambatana na Mtendaji Kijiji Kitama Shuleni, Halmashauri ya Serikali iliyokuwepo Madarakani na ya sasa pamoja na Wazee maarufu Kijijini hapo ambao wote hawakuridhishwa na matumizi ya fedha ya ujenzi wa mradi huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...