Ndugu yetu Dj STEVE B a.k.a Dj Skills anasumbuLiwa na Maradhi ya FIGO, leo tulienda kumjulia Hali' na tulipoingia katika chumba alicholazwa tukapiga Story sana, katikati ya Maongezi alisema, “Mtu ukiwa mzima ni jambo la kumshukuru Mungu sana”, hii ni kutokana na Situation anayopitia.

Steve anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila, natoa Taarifa kwa Marafiki, Wasanii na Wadau wote wa Muziki, wengi hawana TAARIFA, kama tunavyojua Maradhi ya FIGO ni aghali sana.

Sisi kama MaDj/ndugu/marafiki Wenzake tunaangalia Jinsi ya Kushirikiana na Wadau ku-Raise Fund ili kufanikisha aweze kupata Tiba sahihi nje ya nchi, kwani Familia imefika pahala wanahitaji Msaada wa hali na mali.

Wapo waliochangia Matibabu tutawashukuru sana kwa Majina na Tutapeana Taarifa zaidi jinsi ya Kumsaidia mwenzetu Matibabu yake. 

Kwa Mawasiliano Zaidi wasiliana na Kaka yake 0687536015 #RudishaFarajaKwaDjSteve

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...