SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (Unesco) litaendesha mafunzo kwa vituo vya radio 25 nchini Zanzibar kuanzia leo hadi Julai 18 mwaka huu.
Lengo la mafunzo hayo ni kuwezesha waandishi wa habari wa radio na watangazaji kutengeneza vipindi vya maendeleo huku vikizingatia jinsi.
UNESCO itawajengea uwezo waandishi wa habari kuwa na uwezo wa kutengeneza taarifa za habari zenye uhusiano na maendeleo na jinsi.
Aidha radio zote zinazoshiriki zitapatiwa kiasi cha fedha kutumika katika kuboresha uzalishaji wa vipindi na taarifa za habari kwa kuzingatia jinsi na maendeleo kwa muda wa miezi sita.
Lengo kuu la kuboresha vipindi hivyo ni kuwezesha zaidi sauti za wanawake kusikika kupitia vipindi mbalimbali vya mahojiano.
UNESCO kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Uswisi linaendesha mradi wa kuwezesha radio za wananchi kuwa na mifumo ya tehama inayosaidia kutengeneza vipindi vizuri na vyenye kuwezesha maendeleo endelevu nchini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...