Tanzania yadhamiria kupunguza matumizi ya Zabaki kwa wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu kwa asilimia 30% ifikapo 2024. 

Katika kikao cha kupitisha Mpango Kazi wa Taifa wa kupunguza matumizi ya Zebaki kwa wachimbaji wadogo kilichoandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais na kushirikisha sekta husika, leo katika Chuo cha Biashara (CBE) jijini Dodoma, Ikiwa sehemu ya Maandalizi ya utekelezaji wa Mkataba wa Kimataifa wa Minamata ambao Tanzania ipo kwenye mchakato wa kuridhia. 

Zebaki imetajwa kuwa moja kati ya kemikali kumi hatarishi zilizo orodheshwa na Shirika la Afya Duniani na ina madhara makubwa haswa kwenye magonjwa ya mfumo wa fahamu. 

Tanzania inakadiriwa kuwa na wachimbaji wadogo milioni 1.2, asilimia 20-30 ni wachimbaji wanawake ambapo sehemu kubwa ya wachimbaji hawa hutumia zebaki huku kukiwa na makisio ya mwaka ambapo tani 13 mpaka 24 hutumika na huingizwa nchini kinyemela. 

Zaidi ya 25-33% ya wachimbaji wadogo wadogo wameathirika na matumizi ya zebaki,hivyo Serikali imedhamiria kupunguza ama kuondosha matumizi ya zebaki kwa wachimbaji wadogo. 

Wakizungumza mara baada ya kumaliza kikao hicho Bi. Noela R. Magoche ambaye ni mdau wa Madini alisema kuwa zifikiriwe mbinu mbadala kunusuru watoto wanaofanya kazi migodini kwani ndio waathirika wakubwa wa zebaki huku akisisitiza sheria inayokataza ajira kwa watoto 

Kwa upande wake mdau wa Mazingira Bw. Haji Rehani amesema zebaki imetambulika kimataifa kwa madhara makubwa ya kiafya.
Wadau walioshiriki Kikao cha Kupitisha Mpango Kazi wa Taifa wa Kupunguza matumizi ya Zebaki kwa wachimbaji wadogo jijini Dodoma leo. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
………………. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...