Na Woinde Shizza Michuzi Tv,Arusha

Wito umetolewa kwa wanafunzi wa sekondari nchini kuona umuhimu wa kujiandaa wao kwa masomo ya mitaala ya vyuo vikuu watakavyochukuwa wakati wa kujiunga kwa kuwa na uelewa wa masomo watakayoyachagua na kuyachukuwa.

Hayo yamebainishwa na mkuu wa wilaya ya Longido Frank Mwaisumbe kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kwenye ufunguzi wa Maonyesho ya chuo cha Uhasibu kwa wanafunzi wa shule za sekondari 18 za wilaya ya Arusha iliyofanyika chuo hapo jijini Arusha.

Mwaisumbe amesema kujiandaa mapema kunasaidia wanafunzi hao kuzoea mazingira ya masomo ya elimu ya juu kwani wakifanikiwa wanapata uzoefu wa kuzoea fani mbali mbali zinatotolewa na vyuo hivyo.

Amehimiza chuo cha uhasibu kuendeleza maonyesho hayo kwa lengo la kuwaandaa vijana kuweza kufikia ndoto zao za kitaaluma na wasiishie kwenye wilaya ya Arusha pekee na waende mbali zaidi katika mkoa mzima na nchi kwa ujumla.

Awali Mkuu wa chuo cha Uhasibu Prof.Eliamani Sedoyeka amesema kuwa maonyesho hayo yanalengo kubwa la kuwapa nafasi vijana waliopo sekondari kidato cha nne na sita kwa ajili ya kujiandaa kuchukuwa kozi anayopenda itakayomsaida kufikia ndoto zake.

Amesema kwamba maonyesho hayo yatawasaidia wanafunzi hao kukutana na wataalamu na wakufunzi wa chuo hicho pamoja na wanafunzi kujionea taaluma mbalimbali zinazotolewa na chuo hicho na kubadilisha mawazo ya kufikia elimu ya juu.

Amesema kuwa mwisho wa maonyesho hayo wanatarajia kupata wanafunzi wengi watakaopenda kujinga na mafunzo chuo hapo kama lilivyo lengo la chuo hicho na uwepo wake unategemea wanafunzi kuweza kujiendesha.

Maonyesho hayo pia yamelenga namna ya kuanzisha viwanda vidogo vidogo kwa lengo la kuwasaidia vijana kuweza kujiajiri na kutotegemea kuajiriwa jambo litakalosaidia azma ya serikali ya uchumi wa kati wa viwanda.
Mkuu wa chuo cha Uhasibu Prof.Eliamani Sedoyeka pamoja na wa wilaya ya Longido Frank Mwaisumbe wakisikiliza maelekezo ya mwanafunzi wa chuo cha uhasibu Arusha wakati walipotembelea Maonyesho ya chuo cha Uhasibu kwa wanafunzi wa shule za sekondari 18 za wilaya ya Arusha yanayofanyika chuo hapo jijini Arusha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...